Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, June 15, 2012

Mwanzo wa msafara wa Mlima Kilimanjaro

Tarehe 10 Juni 2012 nimemaliza msafara mwingine wa kukwea Mlima Kilimanjaro nikiwa pamoja na kundi la watu 14 katika msafara uliyokuwa na madhumuni ya kuchangisha pesa kwa ajili ya ujenzi wa maktaba ya Shule ya Sekondari Nyegina.

Kutegemea na njia inayotumika, msafara wa kwenda kilele cha Mlima Kilimanjaro unachukuwa kati ya siku 5 hadi 10. Msafara wetu ulichukuwa siku 7 kwenye njia ya Lemosho inayoanzia kwenye lango la Londrossi.
Katika siku ya pili ya msafara, kilele cha Kibo kilionekana mbele yetu kwenye uwanda wa juu wa Shira na kumpa kila mmoja shauku ya kufika kileleni. Wawili kati ya ya 14 tulioanza hawakufanikiwa kufika kileleni. Habari kamili zitawekwa hapa hivi karibuni.

No comments: