Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, September 6, 2011

Lugha yetu Kiswahili


Taswira ya lugha ya Kiswahili na ya wale wanaotumia lugha hiyo ni masuala ambayo yanaleta mitazamo na maana mbalimbali.

Nina rafiki yangu toka Kagera alinisimulia kuwa kwa baadhi ya Wahaya katika nyakati ambazo wenye uwezo wa kuongea Kiswahili fasaha walikuwa wachache, hasa kwenye maeneo ya vijijini, mtu yoyote aliyeongea lugha Kiswahili vizuri alionekana ni mtu mmoja mjanja mjanja ambaye hakuwa mtu wa kuaminika kwa urahisi.

Nakumbuka simulizi nyingine pia toka Uganda zinazoeleza kuwa kwa sababu lugha ya Kiswahili ilikuwa inatumika na wanajeshi (na inaendelea kutumika mpaka sasa) basi lugha hiyo imehusishwa katika historia ya Uganda na nyakati ambapo jeshi lilionekana kama kinara wa ukandamizaji na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Katika matumizi fasaha ya lugha ya Kiswahili, mtu anayeitwa Mswahili, pamoja na kuwa na maana nyingine, ni mtu mwenye maneno mengi, na mjanja.

No comments: