Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, September 11, 2011

Mashambulizi ya Septemba 11: Marekani imeelewa somo?


Leo ni miaka kumi tangu kutokea mashambulizi ya Septemba 11 2011 yaliyofanyika katika miji ya Washington na New York nchini Marekani na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 3,000.

Katika maadhimisho hayo vyombo kadhaa vya habari na taarifa nyingi zilizopo kwenye mtandao zimejikita kwenye kuwauliza walioshuhudia mashambulizi hayo kukumbuka hali ilivyokuwa kwao siku ya shambulio.

Lakini ni sehemu ndogo ya vyombo hivyo vya habari vinavyohoji kwanini shambulio lilitokea, na iwapo sababu ambazo zilisababisha shambulio hilo bado zipo, na ni hatua gani zimechukuliwa kuepuka kutokea tena shambulio kama hilo ambalo lilihusishwa na Osama Bin Laden, ambaye aliuwawa hivi karibuni.

Kama ni kweli kuwa shamubilizi hilo liliongozwa na Osama na wafuasi wake, kuna maswali ya kuuliza. Tofauti za kiitikadi na kidini zinazosemekana zilisukuma mashambulizi hayo bado zipo? Kama zipo, jitihada gani zimefanyika na Serikali ya Marekani na washirika kuziondoa? Kuna uwezekano wa kufikia muafaka utakaoweza kufuta hizo tofauti, na kuzifanya pande zote mbili kusitisha mapambano kati yao?

Afisa mwandamizi wa shirika la ujasusi la Uingereza MI5 alinukuliwa hivi karibuni akisema kuwa uwezekano wa kupambana na kuwashinda wafuasi wa makundi ya Kiislamu kama lile linaolomuunga mkono Osama ni ndogo sana, na nchi za Magharibi sasa zinaangalia uwezekano wa kukubali yaishe, yaani kukaa meza moja na upande wa pili kutafuta suluhisho lisilohusisha matumizi ya nguvu.

Mwandishi mmoja wa Marekani akihojiwa hivi karibuni alisema anaona kama bado Marekani haijajifunza kutokana na mashambulizi ya Septemba 11, 2001. Anaeleza kuwa badala ya kuwa ingefanyika jitihada kubwa ya kujaribu kuelewa tamaduni na desturi za watu wengine duniani, inaonekana kama vile Wamarekani bado wanajiona kuwa wanachoona sawa wao ndiyo sawa kwa binadamu wengine wote na wanaonekana hawajali sana yanayotokea sehemu nyingine ya dunia.

No comments: