Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, September 17, 2011

Mwanaharakati Brian Haw wa Uingereza amefariki

Nilivyotembelea Uingereza mwaka 2006 nilipata fursa ya kumtembelea mwanaharakati Brian Haw, aliyeweka hema mbele ya viwanja vya bunge la Uingereza kwa muda unaokaribia miaka kumi akiishi hapo na kutumia kipaza sauti chake kuendeleza kampeni yake dhidi ya vita vya Irak.
Brian Haw, kushoto, mimi, na mke wake Kay, kulia.
Taarifa ambazo nimechelewa kuzipata zinaeleza kuwa alifariki jijini Berlin, Ujerumani, tarehe 18 Juni, 2011 kutokana na ugonjwa wa saratani ya mapafu.

Nilipomtembelea alinieleza kuhusu kusudio lake la kumfikisha aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Blair kwenye mahakama ya makosa ya kivita kwa kuiingiza Uingereza kwenye vita vya Irak.

No comments: