Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, April 26, 2012

Zawadi ya gari kwa mshindi wa pambano la ngumi za kulipwa kati Francis Cheka na Mada Maugo

Pamoja na zawadi ya fedha taslimu ambazo zitalipwa na promota wa pambano la Jumamosi tarehe 28 Aprili 2012 kati ya Francis Cheka na Mada Maugo, zawadi ya ziada ya gari imeongezwa kwa msindi wa pambano hilo.
Kushoto ni Johannes Lugenge, na kulia ni promota wa pambano, Lucas Rutainurwa, wakionyesha gari atakalozawadiwa mshindi pamoja na mkanda wa ubingwa wa IBF.

Pambano hilo la ubingwa wa mabara wa Afrika ni la raundi 12 na litafanyika kwenye ukumbi wa PTA jijini Dar es Salaam katika uzito wa kilo 75. Kwa mujibu wa taarifa toka kwa promota wa pambano, Lucas Rutainurwa, maandalizi yote yanaenda vizuri.

No comments: