Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, April 25, 2012

Mila na tamaduni

Kwa kabila la Wazanaki ilikuwa desturi kuzika kwenye eneo la nyumbani, mbele ya nyumba anayoishi mfiwa. Ni kwa kufuata mila ndiyo Mtemi Nyerere Burito alizikwa mbele ya nyumbe yake mwezi Aprili 1942. Nyumba ya mviringo inayoonekana kwenye picha ndipo ilipokuwa nyumba yake.
Kaburi la kushoto ni lake, la kulia ni la mke wake wa tano, Christina Mgaya wa Nyang'ombe na mama mzazi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Hata hivyo kwa kufuata mila hizo hizo, mara tu baada ya kuzikwa wakazi wote wa makazi ya mfiwa, hasa kama ni kiongozi wa familia, huhama na kueleka kwenye makazi ambako warithi wa mfiwa waliishi. Hii ni kwa sababu kila mrithi alichukua mali alizorithi na kuhama nazo. Wakati huo, wake za mfiwa pia walirithiwa. Mtemi Nyerere Burito alikuwa na wake 22.

Mila hii ya kuzika eneo la nyumbani inaanza kupotea na kijijini Butiama yapo maeneo ya kuzika.

No comments: