Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, April 18, 2012

Usafiri wa Bajaji


Hakuna ubishi kuwa usafiri wa Bajaji kwenye Jiji la Dar es Salaam ndiyo unaomuwezesha msafiri kusafiri kwa haraka zaidi kati ya sehemu moja na nyingine ya Jiji hilo.

Lakini ni usafiri wenye adha zake. Inasemekana kuwa madereva wa teksi hawafurahii hata kidogo ukweli kuwa Bajaji zimewapoka abiria kwa kiwango kikubwa kutokana na unafuu wa gharama zake na uwezo wake wa kumfikisha mteja anapokwenda kwa haraka zaidi. Kwa hiyo mteja wa Bajaji hayuko salama sana na inasemekana mara kwa mara Bajaji zinagongwa na teksi.

Aidha, inaponyesha mvua Bajaji haina kinga ya kuridhisha kwa msafiri. Hivi karibuni nikiwa Dar wakati mvua ikinyesha nilijikunyata katikati ya kiti cha Bajaji nikijaribu kujikinga na mvua iliyokuwa ikipenya pande zote mbili. Isitoshe, maji ya mvua yalianza kupenya kwenye turubai nikawa kama nimefungulia bomba kwenye bafu manyunyu. Tulipopita kwenye dimbwi la maji gari iliyotupita kwa kasi ilitumwagia maji.

Kila kizuri kina kasoro yake.
posted from Bloggeroid

No comments: