Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, November 10, 2012

Konyagi watoa ala za muziki kwa Msondo Ngoma

Kampuni inayotengeneza kinywaji Konyagi imetoa zawadi ya ala za muziki kwa bendi kongwe ya muziki wa dansi nchini, Msondo Ngoma.
Msondo Ngoma jukwaani.
Akikabidhi hizo ala, Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Distilleries Limited ambao ndiyo watangenezaji wa Konyagi, alisema vifaa hivyo vimetolewa kwa ajili ya kuenzi utamaduni wa Mtanzania na kuiwezesha Msondo Ngoma kuwa imara katika kutoa burudani kwa Watanzania.

Alisema, "Msondo ni bendi kongwe tangu kuanzishwa kwake mwaka 1964. Imesimama imara katika kutoa burudani ya uhakika kwa Watanzania na kutumia nyimbo zake katika kuelimisha, na kufunza jamii ya Watanzania walio wengi."

Alisema kwa kuwapatia vyombo hivyo, Msondo Ngoma itakuwa moto wa kuotea mbali katika kutoa burudani ya uhakika, hali itakofanya bendi nyingine kuwa wasindikizaji katika tasnia ya muziki wa dansi nchini.

Mkurugenzi wa bendi hiyo, Maalim Gurumo, alisema kwa sasa wana deni kubwa kwa Watanzania na kampuni ya Konyagi katika kutoa burudani ya uhakika baada ya kupatiwa vifaa hivyo.
Mkurugenzi wa Tanzania Distilleries Limited David Mgwasa, wa pili kutoka kulia, akikabidhi ala kwa wanamuziki wa Msondo Ngoma.
"Tunaamini baada ya leo kupata vifaa hivi tutatoa burudani ya uhakika sanjari na kukijenga vyema kikosi chetu kwa lengo la kukiimarisha," alisema Gurumo.

Kiongozi wa bendi, Saidi Mabela, alitoa shukurani kwa kampuni ya Konyagi kwa kuwapatia vyombo na aliahidi kuendelea kutoa burudani safi kwa Watanzania na Afrka kwa ujumla.
Habari kamili ziko hapa.

No comments: