Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, November 1, 2012

Mada ya yangu ya leo: aliyeikashifu Kurani aadhibiwe

Kwa hali ya kawaida, mtoto aliyedhalilisha kitabu kitukufu cha dini ya Kiislamu angeweza kuadhibiwa kwa kuchapwa bakora na mzazi wake au kupewa adhabu nyingine nzito ambayo watoto wote wanaokosea hupewa.

Lakini tukio liliotokea siyo la kawaida, kama ambavyo tumeshuhudia madhara yaliyofuata na vurugu zilizotokana na kitendo kile. Makanisa yalivamiwa na mali nyingi kuporwa na kuharibiwa. Uporaji wa mali haufanani hata kidogo na Uislamu kwa hiyo ni dhahiri kuwa katika kundi la watuhumiwa wa matukio haya ambalo linasemekana kuwa ni la waumini wa dini ya Kiislamu walishiriki pia watu ambao hawakusukumwa na hasira ya kudhalilishwa kwa Kurani na dini ya Kiislamu bali ni watu waliyoona fursa ya kuharibu na kupora mali.

Tanzania inayo sheria inayosimamia watuhumiwa ambao wako chini ya umri wa miaka 18. Ni dhahiri hakuna ubishi kuwa huyo mtoto alifanya kosa hilo. Jambo moja ambalo linaweza kuepusha manung'uniko ya dhati ya waumini wa dini ya Kiislamu kulalamikia kile kitendo ni kufikisha suala la yule mtoto mahakamani bila uchelewesho. Kufanya hivyo kutaondoa kabisa kisingizio cha wale ambao wanatafuta fursa ya kufanya fujo kwa kisingizio cha kutetea hadhi na heshima ya dini ya Kiislamu.

Nina hakika yule mtoto tayari anajutia kitendo chake, lakini suala la kutafuta suluhu baina ya waumini wa dini mbalimbali, na suala la kulinda amani nchini linahitaji hatua za kisheria zichukuliwe haraka dhidi yake.

No comments: