Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, November 4, 2012

Lugha yetu Kiswahili

Jana kwenye redio nimesikia marudio ya majadiliano kutoka kwenye vikao vya Bunge la Muungano vinavyoendelea sasa hivi. Alisikika mbunge mmoja, akiwa anatetea hoja kuwa lugha ya Kiswahili itumike kwenye uendeshaji wa shughuli za mahakama, akisema yafuatayo (siyo nukuu halisi kwa maana ya neno kwa neno lakini ni sahihi kwa maana ya nukuu yenyewe):

"...mienendo yote ya shughuli za mahakama iendeshwe kwa lugha ya Kiswahili tu, na kusiwe na option ya Kiswahili au Kiingereza, iwe ni Kiswahili tu."

Anayesisitiza matumizi ya Kiswahili pekee kwenye shughuli za mahakama za Tanzania anajenga hoja yake kwa kutumia neno la Kiingereza.

Ni kazi kweli kweli.

Kwenye kamusi neno option lina maana kadhaa, ikiwa ni pamoja na: uchaguzi, na hiari.

No comments: