Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, February 11, 2013

Mapigano kati ya Wakristu na Waislamu Katoro, Geita, 7 wafa

Kuna taarifa nimepata kuwa watu saba wamekufa kutokana na mapigano kati ya Wakristu na Waislamu huko Katoro, Geita.

Kwa mujibu wa mtoa habari vurugu zilianza kutokana na mmiliki wa bucha kuuza nyama ya ng'ombe aliyechinjwa na Mkristu.

Baadhi ya Waislamu walifika kwenye bucha hiyo na kuichoma moto na kusababisha kuzuka hayo mapigano.

Taarifa zinasema pia kuwa raia wa kigeni ambaye alipita kwenye eneo la vurugu kwa gari alishambuliwa na kuchinjwa.

Hivi karibuni Serikali mkoani Mwanza iliagiza kuwa Waislamu pekee ndiyo waruhusiwe kuchinja wanyama ambao nyama yao inauzwa kwenye bucha.

No comments: