Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, April 30, 2013

Bara la Afrika lapewa sauti kwenye tamasha la filamu la nchini Ubelgiji, Afrika Filmfestival

Mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu nilihudhuria tamasha la filamu nchini Ubelgiji linalojulikana kama Afrika Filmfestival.

Ni tamasha linalofanyika kila mwaka na huhusisha kuonyeshwa filamu nyingi kuhusu bara la Afrika zinazoonyeshwa ndani ya kumbi mbalimbali zilizopo kwenye miji kadhaa ya nchini Ubelgiji.
Bango la Afrika Filmfestival la mwaka huu. Picha: Lilian Nabora. Picha zaidi za Afrkia Filmfestival zinapatikana hapa:  https://www.facebook.com/media/set/?set=a.440201782735019.1073741834.199073470181186&type=1
Madhumuni ya tamasha hilo ni kutoa fursa kwa Waafrika wenyewe kuizungumzia Afrika kwa njia ya filamu za kubuni na zisizo za kubuni. Ni dhahiri kuwa watengeneza filamu wasio Waafrika hawalioni bara la Afrika kwa mtazamo ule ule ambao mzaliwa wa bara hili anaweza kuwa nao. Na aghalabu, mtazamo wa wasiyo Waafrika kuhusu bara la Afrika huwa mara nyingi unatoa taswira ya bara lenye matatizo mengi pasipo mafanikio, jambo ambalo siyo kweli.

Kwenye tamasha la mwaka huu baadhi ya filamu kutoka Tanzania zilizoonyeshwa ni pamoja na The Teacher's Country, filamu isiyo ya kubuni na ambayo nimeshiriki kama mmojawapo wa Watanzania wanne wanaotoa maoni yao kuhusu miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.

Bara la Afrika linapata fursa ya kujisemea nchini Ubelgiji kila mwaka kupitia Afrika Filmfestival.

No comments: