Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, July 7, 2013

Maana ya Mwitongo

Kwa kabila la Wazanaki Mwitongo ni jina la eneo walipoishi watu zamani na kuhama. Ni mahame.
Kwa mila za Wazanaki tukio lililofanya watu wahame eneo ilikuwa kufariki kwa mkuu wa kaya. Baada ya kuzikwa tu mali zake zote (na zama hizo hata wake walikuwa ni mali) zilirithiwa na kuhamishiwa kwa warithi.

Mwitongo kwenye kijiji cha Butiama ni eneo alipoishi na kuzikwa Mtemi Nyerere Burito, baba mzazi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mwalimu Nyerere naye amezikwa eneo hilo hilo tarehe 23 Oktoba 1999.

Chief Nyerere alizikwa tarehe 30 Machi 1942.

No comments: