Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, July 3, 2013

Uchakachuaji mpaka kwenye harusi!

Harusi zimekuwa chanzo cha biashara. Hiyo ni dhahiri. Lakini maharusi wanapokuwa ndiyo watafutaji kwenye harusi yao wenyewe, mipaka ya ustaarabu haipo tena.

Kwa muda mrefu wanakamati kwenye harusi za Tanzania wametumia ushiriki wao kwenye kamati hizo kutoa huduma mbalimbali za kulipiwa zinazohitajika kwenye harusi, kama vile, mapambo, magari, huduma za picha na video, na burudani.

Kwa kawaida kufukuzia huku kwa pesa za sherehe hakuwahusu maharusi wenyewe, wao wakifurahia tu mchango wa ndugu, jamaa, na marafiki wa kwenye kamati kufanikisha sherehe. Leo nimedokezwa kuwa siku hizi baadhi ya maharusi nao wanafanya jitihada kubwa ya kufaidika na harusi zao kwa pesa zinazochangwa.

Bwana harusi mmoja mtarajiwa alimtafuta mtu anayemfahamu na kumwambia afike kwenye kamati ya maandalizi na kutangaza kuwa anatoa huduma ya chakula lakini kwa masharti kuwa faida watagawana na mwenye ndoa. Alisema: "Siwezi kuacha pesa yote hiyo iende kwa watu wengine."

Dada mwingine aliyeolewa hivi karibuni naye inasemekana alipachika watu wake kwenye huduma za mapambo na chakula na kunufaika vizuri baada ya sherehe yake. Naambiwa alikusanya mtaji mzuri wa biashara.

No comments: