Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, July 14, 2013

Mzee Mwinyi alisema kila enzi na kitabu chake?

Alisemaje Mzee Ali Hassan Mwinyi, rais mstaafu wa Tanzania? Kila enzi na kitabu chake?

Sikumbuki vizuri lakini enzi za uongozi wake alitamka maneno yanayofanana na hayo akimaanisha kila rika linafikiwa na matukio au mitazamo ambayo, kwa muda, inachukua umuhimu fulani katika jamii. Halafu baada ya muda yanakuja mengine na yale ya mwanzo yanapoteza umuhimu.
Hili basi la abiria (kwenye picha) lina rangi za timu ya soka ya Uingereza, Manchester United. Na upande wa mbele limeandikwa "Manchester United". Bila shaka mmiliki ni shabiki wa timu hiyo mashuhuri. Linafanya safari zake kati ya Musoma na Bunda.

Nyuma ya basi kuna picha ya mchezaji ambaye sifahamu ni nani na wala simfananishi na mchezaji yeyote mashuhuri ambaye ninamfahamu. Bila shaka wenye enzi zao wanamtambua.

Mimi ingewekwa picha ya Mbaraka Mwinshehe ningemtambua.

No comments: