Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, July 24, 2013

Kazi ya siasa ni chaguo la mwisho kwa mwanafunzi wa shule ya msingi Ramadhani Alfonsi

Mwanafunzi wa shule ya msingi Ramadhani Alfonsi anakusudia kusomea udaktari au urubani. Lakini asipofanikiwa azma ya kufanya mojawapo ya kazi hizo mbili basi ataingia kwenye siasa.

Nimesikia leo mahojiano yake kwenye redio ya TBC FM na ni chaguo ambalo linaibua maswali. Miaka mingi iliyopita nilitembelea shule moja ya sekondari iliyopo Mufindi, Iringa, na mwanafunzi mmoja alipoulizwa angependa kufanya kazi ipi atakapokuwa mtu mzima alisema anataka kuwa mbunge.

Leo hii mwanafunzi Ramadhani anachagua udaktari kwanza, siasa mwisho. Iwapo wanafunzi wengi zaidi sasa wanachagua kazi nyingine kama chaguo la kwanza badala ya kuingia kwenye siasa basi kwa maoni yangu haya ni maendeleo.

Uongozi na siasa vyote vina umuhimu wake lakini naamini kuwa taaluma kama udaktari na taaluma nyingine za ufundi zinaleta manufaa makubwa zaidi kwa jamii kuliko siasa. Kwa mazingira ya sasa kila mtu anaweza kuwa mwanasiasa lakini siyo kila mtu anaweza kuwa daktari, rubani, au mhandisi.

Taarifa nyingine zinazohusiana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2011/07/siasa-ya-tanzania-chama-na-sera-zake-au.html
http://muhunda.blogspot.com/2011/04/mwalimu-wangu-gordian-mukiza.html

No comments: