Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, July 16, 2013

Simba Sports Club wakaribishwa Butiama na Mama Maria Nyerere

Mama Maria Nyerere leo amekuwa mwenyeji wa viongozi na wachezaji wa klabu ya soka, Simba Sports Club kijijini Butiama.
Wageni hao wamepita Butiama wakielekea Musoma ambako kesho wanacheza mechi ya kirafiki.

Baadhi ya viongozi walioongozana nao ni kocha mkuu Abdallah Kibadeni na kocha wa walinda mlango (ambaye alikuwa mwanafunzi mwenzangu Shule ya Sekondari Tambaza) James Kisaka.

Wageni walipata fursa ya kuzuru kaburi la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye amezikwa Butiama.

No comments: