Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, July 11, 2013

Mandhari mpya ya Mwitongo, Butiama

Mandhari ya eneo la Mwitongo inaendelea kupendeza kutokana na kazi ya mtaalamu wa kutengeneza vihenge, Kisyeri Magese.
Kwa miezi kadhaa sasa, mtaalamu huyu asilia kutoka kijiji cha jirani, Nyamuswa, anakarabati na kujenga upya vihenge vya kuhifadhia nafaka ambavyo viko kwenye makazi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwenye eneo la Mwitongo, kijijini Butiama na ambavyo Mwalimu Nyerere alivitumia kuhifadhia ulezi aliolima.

Baadhi ya vihenge, kama kinachoonekana kwenye picha (kulia), vimekamilika na kazi yote inatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2013. Hili ni eneo linalotembelewa na wageni wanaofika Butiama.

No comments: