Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, December 18, 2013

Hatua kumi za mauaji ya kimbari: 7 na 8

Nimetembelea Rwanda hivi karibuni na nikiwa huko nilipata fursa ya kutembelea mojawapo ya vituo vya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Jambo moja la msingi ambalo Watanzania tunaweza kijufunza ni kuwa maafa yaliyotokea Rwanda yanaweza kutokea pia Tanzania. Kwa mujibu wa wachunguzi wa sababu zinozogeuza binadamu mmoja kuwa adui wa binadamu mwenzake na hata kufikia hatua ya kumaliza uhai wa mwenzake ziko duniani kote.

Sababu hizi zinaanza na mchakato wenye hatua nyingi ambao hufikia mauaji kama yale yaliyotokea Rwanda. Kinachozuwia maafa kama hayo kutokea ni hatua mahususi zinazopaswa kuchukulia na jamii za kukatisha uendelezwaji wa huo mchakato.

Kwa mujibu wa Dr. Gregory Stanton wa Genocide Watch, hatua za viashiria vya kuwepo kwa mchakato na za kuzuwia maafa kama ya Rwanda ziko kumi.

Hatua ya Saba: Mipango

Hatua hii inahusisha kuunda mfumo wa kijeshi, kutoa mafunzo kwa wanamgambo, kukusanya silaha za maangamizi, na kuzitawanya kwa wauaji.

Hatua za kuepusha Mipango

Pale inapothibitishwa dalili za mipango kufanyika, basi tahadhari juu ya uwezekano wa kutokea mauaji ya kimabri utolewe. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litowe onyo kuwa litakuwa tayari kuchukua hatua pale tu ambapo lina uhakika kuwa litachukua hatua madhubuti za nguvu dhidi ya wahusika. Viongozi wa dunia wawaonye wale wanaokusudia kutenda maangamizi kuwa watachukuliwa hatua dhidi ya uhalifu watakaoufanya. Msaada wa kibinadamu unadaliwe. Majeshi ya kikanda yaandaliwe na kupewa uwezo wa kujiandaa na wa kifedha.
"Amri Kumi za Gitera" ni waraka uliotolewa na kiongozi wa kabila wa Wahutu kuchochea mauaji ya kabila la Watusi kabla ya mauaji ya kimbari ya Rwanda.  

Hatua ya Nane: Mateso

Katika hatua hii watu wanagawanywa kwa misingi ya ukabila na dini. wahanga wananyang'anywa mali zao. Wahanga hufukuzwa kutoka kwenye nyumba zao. Katika baadhi ya nchi wahanga walihamishwa na kuwekwa kwenye maeneo mahususi ya miji.  Katika baadhi ya nchi wahanga walikusanywa kwenye kambi za wakimbizi wa ndani.

Itaendelea na: 
  • Hatua ya Tisa: Mauaji
  • Hatua ya Kumi: Ukanushaji
Taarifa nyingine zinazohusian na hii:

No comments: