Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, December 20, 2013

Leo kumbukumbu ya kufariki Hayati Alex Nyirenda

Leo ni miaka mitano tangu kufariki Hayati Brigedia Alex Gwebe Nyirenda aliyefariki Dar es Salaam mwaka 2008 kwa ugonjwa wa saratani ya koo.

Usiku wa tarehe 8 Desemba mwaka 1961, muda mchache kabla ya kutimia saa 6:00 kamili usiku, siku ambapo Tanganyika ilipata uhuru wake, Brigedia Nyirenda alikuwa kileleni mwa Mlima Kilimanjaro kupandisha bendera ya taifa jipya la Tanganyika wakati bendera ya Uingereza ilipokuwa inateremshwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Luteni Alex Nyirenda, akiwa na bendera ya Tanganyika na Mwenge wa Uhuru kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro siku Tanganyika ilipopata uhuru wake, tarehe 9 Desemba 1961. (Picha ya Idara ya Habari, Maelezo
Miaka mwili kabla, tarehe 22 Oktoba 1959, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akihutubia Baraza la Kutunga Sheria, alisema yafuatayo:

Sisi watu wa Tanganyika tunataka kuwasha mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilmanjaro umulike nje ya mipaka yetu na kuleta tumaini pale ambapo kulikuwa hakuna matumaini, upendo pale ambapo palikuwa na chuki, na heshima pale 

palipojaa dharau.

Miaka miwili kabla, tarehe 22 Oktoba 1959, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akitoa hotuba kwenye Baraza la Kutunga Sheria, alisema yafuatayo: 
Huu mwenge ambao baadaye ulikuja kujulikana kama Mwenge wa Uhuru ulisimikwa juu ya Mlima Kilimanjaro na Nyirenda, ukiashiria msimamo wa muda mrefu na usiotetereka wa Tanzania kuunga mkono juhudi za ukombozi wa nchi za Kiafrika ambazo katika miaka ya mwanzo ya sitini zilibaki chini ya ukoloni na tawala za kibaguzi.

Mwaka 1958 Nyirenda alikuwa Mtanganyika wa kwanza kuhitimu kutoka Chuo cha Kijeshi cha Sandhurst cha nchini Uingereza. Aidha, kabla ya uhuru, alikuwa Mwafrika wa kwanza kuwa afisa ndani ya Kings African Rifles, jeshi la kikoloni la Uingereza ambalo baada ya uhuru ndiyo likabadilishwa na kuwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Alikuwa na uhusiano wa kiukoo na rais wa zamani wa Zambia, Dk. Kenneth Kaunda, jambo ambalo linakumbusha Waafrika kwamba wako karibu sana kuliko mipaka ya nchi zao inavyoashiria.

No comments: