Isambaze pia kwa wengine.
Thursday, December 24, 2015
Watu kama sisi
Mwaka jana nilishirikishwa kama mmoja wa waliohojiwa kwenye filamu juu ya albino na adha wanazopata kwenye jamii. Inaelimisha vyema.
Isambaze pia kwa wengine.
Isambaze pia kwa wengine.
Tuesday, December 1, 2015
Kufanikisha falsafa ya Sasa Kazi tu! ni kazi kweli kweli!
Tunajifunza mengi kwa kusikiliza. Leo nimemsikiliza mama wa
kijijini Butiama akilalamika kwangu tena kuhusu binti yake kuondoka nyumbani na kuhamia
kwa mtu aliyezaa naye.
Tatizo ni kuwa binti mwenyewe ana umri wa miaka 15 tu, na
aliyempa ujauzito ni mtu mzima. Alimpa hiyo mimba binti akiwa shuleni, na kwa
mujibu wa sheria zilizopo angestahili kuchukuliwa hatua za kisheria. Hayo
hayakutokea.
Nahisi hayakutokea kwa sababu mama wa binti, badala ya
kupeleka hilo suala mbele ya sheria, alifikia makubaliano na huyo jamaa na
inawezekana kuwa alikuwa anapewa pesa ili kutulia.
Sasa leo kalalamika tena kuwa binti karudi kule kule na
akaniambia kuwa sasa anakusudia kufikisha suala hilo polisi. Lakini njia anayotumia
haijanyooka vizuri. Kaniambia kuwa ana jirani yake polisi ambaye amemuomba
aende kumkamatia yule mhalifu.
Jirani yake kakubali lakini amemwambia ampe shilingi elfu
kumi ili amfanyie hiyo kazi. Yeye alisema hana hizo pesa, na akamwambia yule
jirani kuwa amfanyie tu hiyo kazi kwa kuwa wanahusiana pia kiukoo. Jirani polisi
hakusumbuliwa sana na hoja ya uhusiano wa kiukoo, na amemwambia mlalamikaji atafute
angalau shilingi elfu tano ili afanye hiyo kazi.
Miongoni mwa vielelezo kuwa uongozi ni kazi kubwa ni pamoja
na tukio hili. Kwenye ngazi hii ya chini, kujenga imani kuwa falsafa ya Sasa
Kazi tu! itafanikiwa ili mradi yupo rais na waziri mkuu wachapa kazi ni
ndoto tu. Mabadiliko chanya yatapatikana iwapo wote tutashiriki kwa namna
tunavyoweza kuleta mafanikio tunayotarajia.
Wednesday, November 11, 2015
Adha za Mwenge wa Uhuru
Sina tatizo na madhumuni ya mbio za Mwenge wa Uhuru, lakini ninaona kasoro kubwa katika baadhi ya vipengele vya mchakato wa mbio hizo unavyoendeshwa.
Mwenge unapohamishwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine, barabara zote huwa au hazipitiki au zinapitika kwa shida. Barabara zinafungwa mpaka Mwenge upite. Wale wenye shida za dharura wanakuwa hawawezi kutumia usafiri wa barabara kufuatilia shida zao.
Hata mgonjwa mahututi ambaye anapelekwa hospitali au kwenye kituo cha afya anaweza kujikuta ndani ya gari akisubiri Mwenge upite kwanza, ndipo gari alilopanda (kama siyo la kubeba wagonjwa) liweze kuruhusiwa na kuendelea na safari yake.
![]() |
Gari zikiwa zimesimamishwa eneo la Kisesa, Mwanza, zikisubiri msafara wa Mwenge wa Uhuru upite. |
Na isingekuwa vibaya sana iwapo watu wangelazimika kusubiri kwa muda kidogo tu kupisha Mwenge upite. Tatizo ni kuwa wakati mwingine watu husubirishwa kwa muda mrefu sana ili msafara wa Mwenge upite, hata pale ambapo msafara huo unaelekea njia tofauti. Ili mradi tu unapishana nao, basi utalazimika kusimama.
Mwenge wa Taifa ni nembo ya Taifa na nadhani maana ya kusimamishwa watu njiani ni kutoa heshima kwa hiyo nembo ya Taifa. Sijui kama hii ndiyo mantiki ya hatua hizi, lakini inawezekana pia kuwa watu husimamishwa kwa sababu ya kipengele kimoja ambacho nadhani kipo kwenye Sheria ya Usalama Barabarani ambacho kinatamka kuwa msafara rasmi ni lazima upishwe.
Nadhani msafara wa Mwenge unapewa hadhi ya msafara rasmi, kama msafara wa rais au viongozi wengine wa ngazi ya juu. Hatari iliyopo ni kuwa msafara wa Mwenge unaweza kumsubirisha mgonjwa mahututi na asiwahi kupata huduma ya matibabu ambayo inaweza kuokoa maisha yake.
Tuesday, November 10, 2015
Mwalimu Nyerere na nguzo ya uwajibikaji kwa wote katika uongozi
Kwenye kijitabu chake, Ujamaa ni Imani 1: Moyo kabla ya silaha, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anasema:
Yameharibika mengi kwenye nchi hii kwa sababu viongozi wengi wanaamini kuwa uongozi ni sehemu ya kujineemisha wao na familia zao. Na kwa wale ambao hawana ndugu au marafiki kwenye sehemu muhimu za uongozi, uwezekano wa kupata ajira au haupo kabisa au ni finyu sana.
Kurudisha mfumo ambao unatoa fursa sawa kwa wote inawezekana kabisa.
Alinijia Mzanaki mmoja mwaka 1961, mara tu baada ya kupata uhuru. Anataka kazi; anasema, "Mzanaki ndiye Rais, basi sisi Wazanaki tutainuka." Nikamwambia, "Nenda, uko utaratibu wa kupata kazi." Akaniambia, "Na mimi vilevile niende huko?" Nikamwambia, "Kwa nini usiende huko?" Akasema, lazima nije kwako; sasa Mwalimu wewe umekwisha pata, ndugu zako wengine vile vile wapate. Sasa tusipoanza sisi Wazanaki waanze nani? Na wakubwa ndio wa kula, na wakati wa kula umefika; basi tule!"
(Uk. wa 40)
Yameharibika mengi kwenye nchi hii kwa sababu viongozi wengi wanaamini kuwa uongozi ni sehemu ya kujineemisha wao na familia zao. Na kwa wale ambao hawana ndugu au marafiki kwenye sehemu muhimu za uongozi, uwezekano wa kupata ajira au haupo kabisa au ni finyu sana.
![]() |
Mwalimu Nyerere |
Sunday, November 8, 2015
Yanayotokea niliyatabiri
Kwenye makala yangu ya tarehe 14 April 2015 kwenye gazeti la Jamhuri nilitoa maoni yangu juu ya Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015 na kutahadharisha kuwa ni sheria ambayo itawafikisha wengi mahakamani, na hata gerezani.
Na tayari kuna kesi zimeshafikishwa mahakamani dhidi ya watu wanaotuhumiwa kukiuka sheria hii.
Nilitoa hoja kuwa, pamoja na kuwa sheria hii inakusudia kudhibiti uhalifu unaotokea kwa matumizi ya mifumo ya mtandao wa habari na mawasiliano, ni sheria ambayo ina hitilafu kubwa zenye kuhatarisha uhuru wa kusambaza na kutoa maoni mbalimbali ndani ya jamii.
Hakuna raia ambaye analazimishwa kupenda sheria mbalimbali ambazo anaona zina kasoro au hitilafu. Lakini zinabaki kuwa ni sheria na yoyote ambaye hataki, kwa makusudi, kusimama kizimbani kujibu mashtaka ya kukiuka hizo sheria anapaswa kuwa mwangalifu asifike huko.
Njia muafaka ya kuepuka kuishia kubaya ni kuweka mikakati ya pamoja ya kupinga hizi sheria zenye kasoro kwa taratibu zilizopo, za kisheria.
Hoja ya kuwa unawezaje kupinga sheria zenye hitilafu kwa kutegemea serikali ambayo ilipitisha sheria hizi ni hoja yenye nguvu. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania chama tawala kimeshinda uchaguzi kwa asilimia ndogo kuliko kwenye chaguzi zote zilizopita. Mimi naamini kuwa ushindi huo mwembamba unaweza kuleta mabadiliko hata kwa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa tofauti na serikali zake zilizopita, ikawa ni serikali ambayo inasikiliza maoni ya Watanzania na kuanza kupitia upya zile sheria ambazo zinalalamikiwa na watu.
Wasiposikiliza wajiandae kuongeza mahakimu, na kujenga magereza kwa wingi.
Na tayari kuna kesi zimeshafikishwa mahakamani dhidi ya watu wanaotuhumiwa kukiuka sheria hii.
Nilitoa hoja kuwa, pamoja na kuwa sheria hii inakusudia kudhibiti uhalifu unaotokea kwa matumizi ya mifumo ya mtandao wa habari na mawasiliano, ni sheria ambayo ina hitilafu kubwa zenye kuhatarisha uhuru wa kusambaza na kutoa maoni mbalimbali ndani ya jamii.
Hakuna raia ambaye analazimishwa kupenda sheria mbalimbali ambazo anaona zina kasoro au hitilafu. Lakini zinabaki kuwa ni sheria na yoyote ambaye hataki, kwa makusudi, kusimama kizimbani kujibu mashtaka ya kukiuka hizo sheria anapaswa kuwa mwangalifu asifike huko.
Njia muafaka ya kuepuka kuishia kubaya ni kuweka mikakati ya pamoja ya kupinga hizi sheria zenye kasoro kwa taratibu zilizopo, za kisheria.
Hoja ya kuwa unawezaje kupinga sheria zenye hitilafu kwa kutegemea serikali ambayo ilipitisha sheria hizi ni hoja yenye nguvu. Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania chama tawala kimeshinda uchaguzi kwa asilimia ndogo kuliko kwenye chaguzi zote zilizopita. Mimi naamini kuwa ushindi huo mwembamba unaweza kuleta mabadiliko hata kwa serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa tofauti na serikali zake zilizopita, ikawa ni serikali ambayo inasikiliza maoni ya Watanzania na kuanza kupitia upya zile sheria ambazo zinalalamikiwa na watu.
Wasiposikiliza wajiandae kuongeza mahakimu, na kujenga magereza kwa wingi.
Monday, September 21, 2015
Ushauri kwa wanaopiga kura kwa mara ya kwanza
Nimepiga kura kwa mara ya kwanza mwaka 1985. Ningeweza
kupiga kura mwaka 1980 lakini sikuwa nchini wakati huo, nilikuwa masomoni.
Naamini kuna vijana wengi ambao watakuwa wanapiga kura kwa mara ya kwanza mwaka
huu na naomba nitoe ushauri mdogo kwao.
![]() |
Nikiwa na Mwalimu wangu, Godian Muikza (kushoto) ambaye ni diwani anayemaliza muda wake wa Kata ya Ikondo, Wilaya ya Muleba Kusini. |
Hata mwaka huu naamini kuna wapiga kura wengi watajitokeza
wa aina yangu, kama nilivyokuwa mimi mwaka 1985 na kupiga kura kwa kufurahishwa
na jina la mtu tu bila hata kuchambua kwa makini sera anazowakilisha mgombea
huyo. Mwaka 1985 hatukuwa na vyama vingi, lakini sasa vipo. Kwa hiyo, hakuna
sababu ya msingi ya mpiga kura yoyote kuacha kuweka sera za vyama kwenye
mizania na kuamua chama kipi kitapata kura yake. Hatuna uhakika kuwa
yanayoahidiwa yatatekelezwa, lakini bado ni muhimu kuchambua sera tofauti. Akishinda
mtu wako na asipotekeleza ilani yake angalau unayo sehemu ya kuanzia kumhoji.
Kama ulimchagua kwa mkumbo tu hutakuwa na kigezo cha kuamua kuwa hajatimiza
ahadi zake.
![]() |
Wapiga kura wa Butiama wakipiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 |
Pili, nazungumzia wale ambao wana uhakika mkubwa wa matokeo
ya ushindi kwa wanaowaunga mkono, ikiwa ni vyama vya siasa au mgombea mmoja
mmoja. Kusikiliza na kuamini na kauli kama “ushindi ni lazima” ni mwanzo wa kukaribisha
vurugu. Kama kiongozi anatumia kauli hiyo kuhamasisha tu wafuasi wake ili
waweke juhudi kubwa kwenye kampeni inaweza kuwa haina madhara. Lakini kauli hiyo
inaweza kufasiriwa kuwa “tumeshashinda hata kabla ya kupiga kura na mtu yoyote
atakayesema kuwa hatujashinda ni muongo na ametuibia kura.” Hapo tunakaribisha
vurugu.
Mwaka 2010 niliteuliwa wakala wa mgombea ubunge na nilijifunza
kitu kimoja cha msingi. Kama wakala wa mgombea yuko makini, siyo rahisi kuibiwa
kura. Sikulala siku hiyo mpaka matokeo yalipothibitishwa na msimamizi wa
uchaguzi alfajiri ya siku iliyofuata. Wanaoibiwa kura ni wale ambao wameweka
mawakala ambao siyo waaminifu au ambao hawakuwa makini. Mtu akitaka kuibiwa,
ataibiwa.
Tangu kuanzishwa mfumo wa vyama vingi tumesikia shutuma kuwa
Chama cha Mapinduzi (CCM) ndiyo wataalamu wa kuiba kura. Kama hizo shutuma ni
za kweli, sioni sababu yoyote ya kutoana roho kwa sababu sasa hivi Mhe. Edward
Lowassa amehamia upande wa pili. Yeye amekulia na kujifunza siasa ndani ya CCM na,
kwa vyovyote vile, atakuwa amehama na uelewa uliobobea wa mbinu zinazotumika
kuiba kura na atakuwa anafahamu mbinu za kutumika kuzuwia wizi huo. Mwizi
hawezi kumuibia mwizi.
Mwanachama wa Chama cha wananchi (CUF) akielekea kwenye mkutano wa kampeni jijini Mwanza mwaka 2010. |
Kwa sababu hii sioni kabisa busara ya mtu yoyote kutamka
kuwa kaibiwa kura kama yeye mwenyewe hataki kuibiwa kura. Labda atumie kauli hiyo
kama kisingizio cha kupinga matokeo. Tunao wajibu wa kujenga mazingira yenye kulinda
amani, lakini tunao pia uwezo wa kuweka mazingira yanayobomoa amani.
Uchaguzi huu umeibua ushindani mkubwa kati ya CCM na vyama
vinavyowakilishwa na UKAWA. Kwa bahati mbaya, ushindani unaonyesha dalili za
uhasama na muelekeo kuwa kipindi hiki cha kampeni kitaibua matukio ya kuvunjika
kwa amani. Lakini amani itavunjika tu iwapo wapiga kura tutakubali ivunjike. Na
amani inapovunjika hutasikia hata siku moja kuwa Mhe. John Magufuli au Mhe.
Edward Lowassa kavunjika mguu kwa sababu ya vurugu za kisiasa.
Bado sijaona sababu ya msingi ya kuvunjika kwa amani
kutokana na uchaguzi. Usikubali kuwa chanzo cha kuvunjika kwa amani.
Thursday, September 10, 2015
Mada yangu ya leo: Hii siyo siasa
Tuawasikia baadhi ya viongozi waandamizi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakimtaka mgombea urais wa UKAWA akubali wakutane kwenye mdahalo ili waeleze maovu yake. Yeye anasema kama wana ushahidi kuhusu maovu yake waende mahakamani. Hii siyo siasa.
Nionavyo mimi, siasa ingekuwa hivi:
1. Kama una tuhuma dhidi ya mgombea urais husubiri awe rais kwanza. Unasema yale unayoyafahamu. Akisha kuwa rais halafu utafanya nini? Utaomba mdahalo?
2. Mpiga kura ana haki ya kufahamu taarifa zote muhimu juu ya wagombea kabla hajafikia uamuzi wa kumchagua yule ambaye anaona anafaa. Kuamua kuwa taarifa hizo ni kama mali adimu haina tofauti na kujifanya mtaalamu wa bishara (au taaluma nyingine) ambaye ametumia muda mwingi kupata elimu na uzoefu kwenye taaluma yake halafu anaamua, kwa haki kabisa, kuwa taarifa hizo hazitoki mpaka kwa masharti yanayomnufaisha yeye, au kwa pesa au kwa njia nyingine atakayoamua. Ni wajibu wa kiongozi yoyote makini kumpa mpiga kura taarifa sahihi, hasa wakati wa uchaguzi.
3. Mpaka sasa, tumemsikia mtuhumiwa akisema kuwa hana tuhuma yoyote na, kwa mantiki hiyo, anaposema nendeni mahakamani ni sawa kabisa. Wale wenye taarifa hizo wakaziibue mahakamani. Watuhumiwa wachache sana hukubali kosa nje ya mahakama.
Kwa hayo machache, sisemi kuwa tuhuma ni za uongo.
Ninachoona ni kundi moja ambalo limekosa ujasiri wa kutamka wanalotaka kutamka na badala yake kuwafanya wapiga kura kubaki wanabishana wenyewe kwa wenyewe na ujinga wao* (kama ujinga huo upo kweli) bila kuwapa taarifa ambazo zinaweza kuwasaidia kufanya chaguo sahihi.
Kama huo ujasiri unakosekana, basi ni bora kunyamaza tu. Kuwafanya wapiga kura kuwa wajinga mara ya pili ni hatari kisiasa.
Huo ndiyo ujumbe wango leo hii.
*Wale ambao mtakimbilia kwenye Tume ya Mawasiliano kunilalamikia kuhusu kutumia neno "ujinga" ni kwamba siyo tusi, ni hali ya kutofahamu tu.
Nionavyo mimi, siasa ingekuwa hivi:
1. Kama una tuhuma dhidi ya mgombea urais husubiri awe rais kwanza. Unasema yale unayoyafahamu. Akisha kuwa rais halafu utafanya nini? Utaomba mdahalo?
2. Mpiga kura ana haki ya kufahamu taarifa zote muhimu juu ya wagombea kabla hajafikia uamuzi wa kumchagua yule ambaye anaona anafaa. Kuamua kuwa taarifa hizo ni kama mali adimu haina tofauti na kujifanya mtaalamu wa bishara (au taaluma nyingine) ambaye ametumia muda mwingi kupata elimu na uzoefu kwenye taaluma yake halafu anaamua, kwa haki kabisa, kuwa taarifa hizo hazitoki mpaka kwa masharti yanayomnufaisha yeye, au kwa pesa au kwa njia nyingine atakayoamua. Ni wajibu wa kiongozi yoyote makini kumpa mpiga kura taarifa sahihi, hasa wakati wa uchaguzi.
3. Mpaka sasa, tumemsikia mtuhumiwa akisema kuwa hana tuhuma yoyote na, kwa mantiki hiyo, anaposema nendeni mahakamani ni sawa kabisa. Wale wenye taarifa hizo wakaziibue mahakamani. Watuhumiwa wachache sana hukubali kosa nje ya mahakama.
Kwa hayo machache, sisemi kuwa tuhuma ni za uongo.
Ninachoona ni kundi moja ambalo limekosa ujasiri wa kutamka wanalotaka kutamka na badala yake kuwafanya wapiga kura kubaki wanabishana wenyewe kwa wenyewe na ujinga wao* (kama ujinga huo upo kweli) bila kuwapa taarifa ambazo zinaweza kuwasaidia kufanya chaguo sahihi.
Kama huo ujasiri unakosekana, basi ni bora kunyamaza tu. Kuwafanya wapiga kura kuwa wajinga mara ya pili ni hatari kisiasa.
Huo ndiyo ujumbe wango leo hii.
*Wale ambao mtakimbilia kwenye Tume ya Mawasiliano kunilalamikia kuhusu kutumia neno "ujinga" ni kwamba siyo tusi, ni hali ya kutofahamu tu.
Tuesday, September 8, 2015
Wednesday, August 12, 2015
Lugha yetu Kiswahili: Kiswahili kinasambaa toka Scotland mpaka Butiama
Wanafunzi 12 toka Chuo Kikuu cha Edinburgh wapo kijijini Butiama kujifunza Kiswahili kwa mwezi mmoja.
Mafunzo yao ni sehemu ya mpango wa Chuo Kikuu cha Edinburgh kuvutia wanafunzi kutoka nje ya Scotland kujiunga na masomo mbalimbali katika chuo hicho maarufu, ambacho mmoja wa wanafunzi wake mashuhuri ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Wanafundishwa Kiswahili na walimu Watanzania watatu.
Kuwepo kwa wanafunzi wa lugha ya Kiswahili kutoka Edinburgh hapa Butiama kwa Mwalimu Nyerere, ambaye pia anatambuliwa kama mmoja wa viongozi wa Tanzania ambao walitoa mchango mkubwa katika kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili ni suala la fahari kubwa kwa mmoja wa waratibu wa mafunzo haya ya Kiswahili, Dk. Thomas Molony, ambaye mwaka jana alichapisha kitabu juu ya maisha ya Mwalimu Nyerere kinachoitwa Nyerere: The Early Years.
Akiwa Butiama wakati akifanya utafiti wa kitabu chake, nilipata fursa ya kuchangia kwa kiwango kidogo taarifa ambazo hatimaye alizitumia kwenye kitabu hicho.
Na mimi nakubaliana naye. Naamini kuwa Mwalimu Nyerere angekuwa hai angefurahi sana kushuhudia wanafunzi kutoka chuo chake cha zamani wakiwa Butiama kujifunza lugha ambayo yeye mwenyewe aliipenda na aliyoshiriki kuiimarisha.
Mafunzo yao ni sehemu ya mpango wa Chuo Kikuu cha Edinburgh kuvutia wanafunzi kutoka nje ya Scotland kujiunga na masomo mbalimbali katika chuo hicho maarufu, ambacho mmoja wa wanafunzi wake mashuhuri ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Wanafundishwa Kiswahili na walimu Watanzania watatu.
![]() |
Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Edinburgh wakiwa Butiama, pamoja na walimu wao wa lugha ya Kiswahili. |
Akiwa Butiama wakati akifanya utafiti wa kitabu chake, nilipata fursa ya kuchangia kwa kiwango kidogo taarifa ambazo hatimaye alizitumia kwenye kitabu hicho.
Na mimi nakubaliana naye. Naamini kuwa Mwalimu Nyerere angekuwa hai angefurahi sana kushuhudia wanafunzi kutoka chuo chake cha zamani wakiwa Butiama kujifunza lugha ambayo yeye mwenyewe aliipenda na aliyoshiriki kuiimarisha.
Tuesday, July 14, 2015
Kwenye mchakato huu, dozi ya politiki ilizidi kiwango
Nafikiri ni General Defao aliyeimba: "umekalia politiki tu, kazi hufanyi". Katika kipindi ambacho Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikiendelea na mchakato wa kupata mgombea urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu, hali hiyo ya kukalia politiki tu imekuwa kweli kwa watu wengi.
Wengi tunatambua umuhimu wa mchakato wowote wa kisiasa kama jambo muhimu katika jamii na jambo la msingi ni kupata viongozi wanaosimama kuwakilisha matakwa ya wengi. Na bila shaka ni suala ambalo kila mmoja wetu anapaswa kulifuatilia kwa karibu sana.
Lakini mchakato huo unapotufanya tuache kila kitu, hata zile kazi ambazo zinatulipa ajira, basi suala la siasa linakuwa limezidi dozi ya kawaida. Kuna watu wengi tu ambao hawakuwa na nafasi yoyote katika vikao vya maamuzi vya CCM vilivyokaa Dodoma kumpitisha John Magufuli ambao walienda Dodoma kufuatilia mchakato huo.
Baadhi ya ambao hatukuwa Dodoma tulikaa muda wote tukisikiliza taarifa kwenye vyombo vya habari kufuatilia mchakato. Wengine wengi walitumia muda wao kujibishana na wenzao kwenye mitandao ya jamii. Dozi haikuwa ndogo hata kidogo.
Naamini watafiti wanaweza kubaini kushukua kwa uzalishaji katika kipindi cha majuma kadhaa yaliyopita.
Tushukuru kuwa mchakato huu wa CCM umeisha na labda watu watarejea kwenye maisha yao na majukumu yao ya kila siku.
Wengi tunatambua umuhimu wa mchakato wowote wa kisiasa kama jambo muhimu katika jamii na jambo la msingi ni kupata viongozi wanaosimama kuwakilisha matakwa ya wengi. Na bila shaka ni suala ambalo kila mmoja wetu anapaswa kulifuatilia kwa karibu sana.
Lakini mchakato huo unapotufanya tuache kila kitu, hata zile kazi ambazo zinatulipa ajira, basi suala la siasa linakuwa limezidi dozi ya kawaida. Kuna watu wengi tu ambao hawakuwa na nafasi yoyote katika vikao vya maamuzi vya CCM vilivyokaa Dodoma kumpitisha John Magufuli ambao walienda Dodoma kufuatilia mchakato huo.
Baadhi ya ambao hatukuwa Dodoma tulikaa muda wote tukisikiliza taarifa kwenye vyombo vya habari kufuatilia mchakato. Wengine wengi walitumia muda wao kujibishana na wenzao kwenye mitandao ya jamii. Dozi haikuwa ndogo hata kidogo.
![]() |
Baadhi ya watia nia waliofikia hatua za mwisho za mchakato wa kupata mgombea urais wa CCM |
Tushukuru kuwa mchakato huu wa CCM umeisha na labda watu watarejea kwenye maisha yao na majukumu yao ya kila siku.
Monday, June 22, 2015
Utamaduni wa utoaji majina miongoni mwa kabila la walango wa Uganda
Nimepata fursa hivi karibuni ya kuonana tena na mmoja wa watoto wa kiume wa rais wa zamani wa Uganda, Apollo Milton Obote na tuliongelea utamaduni wa kutoa majina kwa kabila lao la walango.
Nilipenda kufahamu kwa nini jina lake halina ubini wa baba yake, Obote. Yeye anaitwa Eddy Engena-Maitum, na ni askofu wa kanisa la Bright Morningstar Ministry. Alinijibu kuwa kwa mila na desturi za kabila lao, kila mtoto anayezaliwa anapewa majina yake bila kuweka jina la baba mzazi. Alifafanua kuwa majina yote ya baba yake ni yake, hakutumia ya baba yake (babu yake Eddy).
Mdogo wake naye anafuata utaratibu huo huo: ni Jimmy Akena, ambaye ni mwanasiasa na rais wa chama cha Uganda Peoples' Congress. Aidha, ametangaza nia ya kugombea nafasi ya urais kupitia chama chake kwenye uchaguzi mkuu wa Uganda utakaofanyika 2017. Alipomuoa mbunge mwenzake Betty Amongi mwaka 2013 Rais Yoweri Museveni alihudhuria harusi hiyo.
Eddy anafafanua kuwa zipo faida na hasara za kutotumia ubini wa baba yao. Wakati mwingine akijitambulisha kama mtoto wa Milton Obote wale wasiomfahamu humtilia shaka wanapoona kuwa jina lake kamili halina jina la baba yake. Faida ni kuwa pale inapokuwa siyo lazima kujitambulisha hivyo inampa fursa ya kubaki bila utambulisho huo ambao, kwa watoto ambao wazazi ni wanasiasa inaweza kuwa ni jambo linalozua hisia tofauti kwa wanaobaini hali hiyo. Inaweza kutokea kubebeshwa kesi ambayo siyo yako.
Nilipenda kufahamu kwa nini jina lake halina ubini wa baba yake, Obote. Yeye anaitwa Eddy Engena-Maitum, na ni askofu wa kanisa la Bright Morningstar Ministry. Alinijibu kuwa kwa mila na desturi za kabila lao, kila mtoto anayezaliwa anapewa majina yake bila kuweka jina la baba mzazi. Alifafanua kuwa majina yote ya baba yake ni yake, hakutumia ya baba yake (babu yake Eddy).
Mdogo wake naye anafuata utaratibu huo huo: ni Jimmy Akena, ambaye ni mwanasiasa na rais wa chama cha Uganda Peoples' Congress. Aidha, ametangaza nia ya kugombea nafasi ya urais kupitia chama chake kwenye uchaguzi mkuu wa Uganda utakaofanyika 2017. Alipomuoa mbunge mwenzake Betty Amongi mwaka 2013 Rais Yoweri Museveni alihudhuria harusi hiyo.
![]() |
Mimi (kulia), nikiwa pamoja na Askofu Eddy Engena-Maitum jijini Kampala hivi karibuni. |
Monday, April 13, 2015
Hapa ndipo alipozaliwa Mwalimu Nyerere
Hapa ndipo miaka 93 iliyopita alizaliwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kijijini Butiama.
Ni eneo la Mwitongo alipoishi baba yake Mtemi Nyerere Burito wa kabila la Wazanaki wa eneo la Butiama, na mama yake, Mgaya wa Nyang'ombe, aliyekuwa mke wa tano kati ya wake 22 wa Mtemi Nyerere.
Leo eneo hili ni sehemu inayotembelewa na mamia ya wageni kila mwezi kutoka sehemu mbalimbali.
Ni eneo la Mwitongo alipoishi baba yake Mtemi Nyerere Burito wa kabila la Wazanaki wa eneo la Butiama, na mama yake, Mgaya wa Nyang'ombe, aliyekuwa mke wa tano kati ya wake 22 wa Mtemi Nyerere.
Leo eneo hili ni sehemu inayotembelewa na mamia ya wageni kila mwezi kutoka sehemu mbalimbali.
Saturday, March 14, 2015
Mahojiano yangu kuhusu wagombea urais
Majuma kadhaa yaliyopita nilihojiwa na mwandishi wa habari wa Mwanza kuhusu maoni yangu juu ya wagombea urais waliojitokeza kuwania nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu.
Sehemu ya mahojiano hayo imechapishwa hapa.
Sehemu ya mahojiano hayo imechapishwa hapa.
Saturday, January 24, 2015
Waheshimiwa wengi sana Tanzania
Neno mheshimiwa limekosa heshima inayokusudiwa kwa maoni yangu.Sababu kubwa ni kuwa Tanzania ina waheshimiwa wengi sana.
Sizungumzii wale watu ambao nafasi zao katika jamii zinatulazimu kuwaita "waheshimiwa", kwa mfano mahakimu, majaji, na wabunge. Nazungumzia tabia iliyojengeka ya matumizi ya "mheshimiwa" kwa kila raia anayezungumza Kiswahili.
Mimi nilidhani kuwa madhumuni ya kutumia "mheshimiwa" haina tofauti sana na kumuita mtu daktari. Madhumuni ni kumpambanua kama mtu mwenye nafasi muhimu katika jamii ambayo inahitaji kuweka mipaka ya namna watu wengine wanavyowasiliana nae, au kubainisha kuwa ni mtu ambaye anayo taaluma maalum. Kwa upande wa majaji na mahakimu ni viongozi ambao wana majukumu muhimu ndani ya jamii na wanapata upendeleo fulani kwa namna wanavyochukuliwa na jamii. Kwa kuwapa huo upendeleo jamii pia inategemea kuwa waheshimiwa watakuwa watu wanaojiheshimu mbele ya jamii.
Sasa cheo hiki anapopewa kila mtu kuna hatari ya kukigawa kwa watu ambao hawajiheshimu hata chembe na ambao wataharibu maana halisi ya uheshimiwa. Kwa maoni yangu waheshimiwa wanaosimamia kesi mahakamani ndiyo wanastahili zaidi kuitwa waheshimiwa.
Sisi tuliobaki tungerudia kuitana ndugu, ingawa wengi wanaamini undugu unahusiana na siasa ya Ujamaa peke yake. Siyo kweli. Tumsikilize Rais Mstaafu Mkapa, akizungmuza kwenye semina ya Muafaka ya Vyama vya Siasa, Zanzibar, tarehe 7 Machi 2005:
"Ndugu siyo neno la kiitikadi tu, linahusu pia utamaduni wetu. Mtaniwia radhi nikiwaita "Ndugu wanasemina."
Wewe ni ndugu au mheshimiwa?
Sunday, January 11, 2015
Kandambili, rangi mbili
Sehemu nyingi za Tanzania, hasa kwenye miji midogo, ukiingia kwenye gesti au hoteli basi kama umewekewa kandambili chumbani utakuta kila moja ina rangi tofauti.
Sababu kubwa ni kuwa baadhi ya wateja wanaoingia kwenye sehemu hizi siyo waaminifu na wanapoondoka huamua kuondoka na kandambili. Inaaminiwa kuwa zikiwa zina rangi mbili tofauti basi mwenye kusudio la kuziiba ataacha kufanya hivyo. Sina hakika kama inasaidia kuzuwia wizi.
Subscribe to:
Posts (Atom)