Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, March 22, 2010

CCM yaendeleza rirandi* ughaibuni

Hizi taarifa zilichelewa kunifikia, lakini siyo vibaya kuzitoa.

Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Pius Msekwa alizuru Uingereza hivi karibuni ambapo alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe za kuadhimisha miaka 33 ya CCM zilizoandaliwa na jumuiya ya wana-CCM waliyoko Uingereza.

Katika sherehe hizo alikabidhi kadi za uanachama kwa wanachama wapya pamoja na kutoa vitendea kazi kwa viongozi wa mashina ya CCM yaliyoanzishwa huko.

Baadhi ya mambo aliyozungumzia huko, kwa mujibu wa taarifa niliyopata kutoka kwa waandaaji, ni pamoja na Azimio la CCM la Zanzibar. Kwa mujibu wa taarifa hiyo:
"Alisema Azimio la Zanzibar la Februari 1991 halikuvunja Azimio la Arusha isipokua lilitazama upya masharti ya uanachama wa CCM na hasa ibara ya 8(7) ya katiba ya CCM toleo la 1987. Azimio la Zanzibar liliondoa miiko ya uongozi iliyowabana halaiki ya wanachama walio wakulima na wafanyakazi wa kawaida hasa baada ya mabadiliko ya uchumi na siasa ya vyama vingi. Hivyo alionya kuwa CCM na serikali yake haitawavumilia watovu wa maadili wanaokighilibu Chama na kuhujumu uchumi kwa kutumia mwanya wa CCM kujisahihisha, kujiboresha na kujiiimarisha."

 Picha zote zinaonyesha matukio mbalimbali wakati wa sherehe/mkutano huo.


*Kuhusu Rirandi: Baada ya rafiki yangu DC wa Tegeta kuendeleza libeneke kwa muda mrefu kwenye Michuzi Blog nimeona na mimi sina budi kumuunga mkono kwa mazingira ya eneo ninaloishi hivi sasa. Hivi karibuni nilitembelea blogu ya rafiki yangu John Kitime na kujifunza maana ya neno "libeneke." Inasemekana ni mtindo wa ngoma ya asili ya kabila la Wapogoro kutoka mkoa wa Mororgoro.

Mimi badala ya kutumia "libeneke", naendeleza "Rirandi." Wenyeji wa mkoa wa Mara watafahamu kuwa Rirandi ni ngoma ya asili ya kabila la Wakurya.

No comments: