Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, March 29, 2010

Ziarani Uingereza

Picha: Mwenyeji wangu, Anna, Dk. William Shija, na mimi kwenye ofisi ya Dk. Shija.

Picha hii ya zamani kidogo inatokana na ziara niliyofanya nchini Uingereza mwaka 2007 kufuatia mualiko niliyopata toka Global Women's Strike, kikundi cha wanaharakati wa Uingereza wanaotetea haki za wanawake.

Wakati wa ziara hiyo nilipata fursa ya kumtembelea Dk. William Shija, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola kwenye ofisi yake iliyopo jirani na bunge la Uingereza. Dk. Shija alikuwa mmojawapo wa wagombea waliojitokeza ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania uteuzi wa kuwa mgombea urais wa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2005. Wakati huo alikuwa mbunge wa Jimbo la Sengerema.

Amewahi kuongoza wizara ya Sayansi, Teknolojia, na Elimu ya Juu; Wizara ya Habari na Utangazaji; Wizara ya Nishati na Madini; na Waizara ya Viwanda na Biashara.

Dk. Shija aliteuliwa tarehe 9 Septemba 2009 kushika wadhifa wake wa sasa kwa kipindi cha miaka mitano.

No comments: