Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, March 15, 2010

Kuhusu Mwitongo

Eneo la Butiama linalojulikana kama Mwitongo ni sehemu yalipokuwa makazi ya Mtemi Nyerere Burito wa kabila la Wazanaki, ambaye alitawala kati ya mwaka 1912 - 1942. Alifariki tarehe 30 Machi 1942 na kuzikwa hapo hapo Mwitongo.

Maana ya Mwitongo ni mahame, au sehemu walipoishi watu na kuhamia sehemu nyingine. Sababu kubwa ya kuhama eneo ilikuwa kufariki kwa kiongozi mkuu wa familia (au ukoo) na kurithiwa kwa mali zake. Warithi walichukuwa mgao na kuhamia kwenye makazi yao. Enzi hizo, wake pia walirithiwa kwa hiyo wengi wa wake 22 wa Mzee Nyerere walirithiwa na kuhamia maeneo mengine.

Picha: Kaburi la Mtemi Nyerere Burito (kushoto), na la mke wake wa tano Mgaya wa Nyang'ombe (kulia). Nyumba ya mviringo ndipo ilipokuwa nyumba ya Mtemi Nyerere

Mgaya wa Nyang'ombe alikuwa mke wa tano wa Mtemi Nyerere, lakini tunaambiwa hakurithiwa kwa sababu mwanae, Julius Kambarage, alitamka angemtunza mama yake. Wageni wanaotembelea Mwitongo huonyeshwa eneo ambapo ilikuwepo nyumba ya Mgaya, au sehemu alipozaliwa Mwalimu Nyerere.

Picha: Sanamu ya Mwalimu Nyerere iliyopo Mwitongo, sehemu alipozaliwa.

Kabla ya kufariki, Mwalimu Nyerere alielekeza sehemu ambapo angependa kuzikwa, pembeni tu ya sehemu alipozaliwa. Haikuwezekana kumzika alipotamka kwa sababu ni sehemu ambayo ulijengwa mfereji wa maji machafu. Sehemu iliyochaguliwa baadaye haikuwa mbali na eneo aliloelekeza yeye.

 Picha: Nyumba iliyojengwa kuzungukia kaburi la Mwalimu Nyerere, eneo la Mwitongo, Butiama.

No comments: