Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, June 7, 2011

'Chanzo' cha Mto Nile


Mwaka jana nilipata fursa ya kutembelea Uganda na kufika kwenye ‘chanzo’ cha Mto Nile unaotokana na Ziwa Viktoria na kupita nchi kadhaa, ikiwa ni pamoja na Sudan, na Misri, kabla ya kuingia kwenye Bahari ya Mediterranean.
Kutoka kushoto, Samwel Muganda, mimi, mgeni toka Misri, Francois Lumumba (mwanae marehemu Patrice Lumumba), na wageni wawili kutoka Misri ambao majina yao hayakuweza kupatikana, tulipotembelea Jinja wakati wa sherehe za uhuru wa Uganda.
Tafsiri ya meneno kwenye bango lililopo kwenye picha ni:
KARIBU KWENYE CHANZO CHA MTO NILE  JINJA, UGANDA
Sasa uko kwenye kingo ya mashariki ya Mto Nile, kwenye sehemu ambapo mto unaanza kutiririka kutoka Ziwa Viktoria (chanzo cha Nile) kuelekea kwenye Bahari ya Mediterranean. Inachukuwa miezi mitatu kwa maji kumaliza safari ya maili 4,000 (kilomita 6,400).

Maporomoko ambayo John Hanning Speke aliyaona mwaka 1862 na kuyaita “Maporomoko ya Rippons” ikiwa ni jina la rais wa Royal Geographical Society (Chama cha kifalme cha wanajiografia) cha London yalifunikwa na maji mwaka 1947 kufuatia ujenzi wa bwawa kubwa la Owen Falls. Bwawa lilimalizika kujengwa mwaka 1952 likifanikiwa kutumia kasi ya maji kutoka kwenye Ziwa kufua umeme kwa njia ya maji kwa ajili ya Uganda.

“Omugga Kiyira” ni jina la asili la Mto Nile. Ghuba iliyopo nyuma ya bango hili, sehemu ambapo maji ya Ziwa Viktoria yanajipenyeza ndani ya Mto Nile, inaitwa Ghuba ya Napoleon.

Kwenye kingo ya magharibi ya mto kuna mnara mrefu wenye pango mraba zilizochongwa juu kwenye sehemu ambapo Speke alisimama kwa saa nyingi alipoona chanzo cha Mto Nile, na kufanya pajulikane kwa ulimwengu wa nje.
Mimi najiuliza swali. Ziwa Viktoria linapokea maji kutoka mito mbali mbali ya nchi za Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Mto Mara wa Tanzania, na Mto Kagera unaopita Rwanda, Burundi, na Tanzania. Maji yote haya kutoka mito kadhaa yanachangia maji yanayoingia kwenye Mto Nile. Itakuwaje chanzo kiwe Jinja tu? Labda ingekuwa sahihi kusema kuwa kuna vyanzo vingi vya Mto Nile ambavyo vimetapakaa kwenye nchi za Afrika Mashariki.

No comments: