Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, June 20, 2011

Mlima Meru, wa pili kwa urefu Tanzania, wa 72 ulimwenguni

Mlima Meru ni Mlima wa pili kwa urefu Tanzania baada ya Mlima Kilimajaro. Una urefu wa mita 4,565 juu ya usawa wa bahari na unaorodheshwa kushika nafasi ya 72 kwa milima mirefu kuliko yote duniani. Mlima Meru uko mkoa wa Arusha, ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Arusha.
Mlima Meru ukionekana kutoka Arusha.
Watu wengi wanaoparamia milima kama mimi huanza kupanda milima rahisi kwanza kabla ya kwenda kwenye ile yenye kutoa changamoto kubwa zaidi. Wengi hupanda Mlima Meru kabla ya Kilimanjaro, ingawa mimi nimeanza kupanda Mlima Kilimanjaro nikikusudia baadaye kuukabili Mlima Meru. Waliopanda milima yote miwili wanasema kuwa, pamoja na kuwa Meru siyo mrefu kuliko Kilimanjaro (Kilimanjaro una urefu wa mita 5,895 juu ya usawa wa bahari), untoa changamoto kali kwa sababu kupanda kwake ni mpando wa siku 2 mfululizo wakati Mlima Kilimanjaro unahusisha njia zinazovuka mabonde kadhaa na hiyo ina maana kuwa wanaoelekea kileleni hujikuta wakipanda na kushuka na hata wakati mwingine kupita sehemu zenye tambarare.

Tafiti zinathibitisha kuwa miaka bilioni kadhaa iliyopita Mlima Meru ulilipuka kutokana na msukumo wa gesi za volkano na kusababisha sehemu yake ya pembeni kumeguka na kutapakaa kwenye eneo la umbali unaofikia upande wa magharibi ya Mlima Kilimanjaro. Hizo tafiti zimethibitisha kuwepo tabaka ya udongo wa Mlima Meru juu ya sehemu hiyo ya Mlima Kilimanjaro.

Picha hii ya chini ambayo imepigwa na vyombo vinavyoruka juu vya shirika la Marekani NASA inaonyesha vizuri sehemu ya Mlima Meru iliyomeguka kutokana na mlipuko wa volkano. Tofauti ya rangi iliyopo kwenye picha inaakisi tofauti ya umbali kutoka usawa wa bahari wa eneo hilo la Mlima Meru.
Hii picha ya Mlima Meru inatumika kwa hisani ya NASA/JPL-Caltech. [Photo: Courtesy NASA/JPL-Caltech]

No comments: