Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, June 13, 2011

Omukama wa Missenyi

Mapema mwaka huu, nikiwa kwenye ziara ya Mkoani Kagera, nilipata fursa ya kutembelea Bunazi, katika Wilaya ya Missenyi na kuzuru makazi ya mtemi wa eneo hilo. Mtemi wa sasa wa Missenyi, tangu mwaka 2001, ni Omukama Paulo Lwamujongo II, aliyemrithi baba yake, Omukama Serapion N.L. Kyamukuma II (1932 – 2001) aliyetawala kati ya mwaka 1955 hadi 2011 alipofariki.

Orodha ya watawala waliyomtangulia Omukama Paulo Lwamujongo II
Na.
Jina
Maelezo
Kipindi cha Utawala (kama ni wazi, miaka haijulikani)
1
Wakara
Bunyoro

2
Kagoro I
Alitoka Bunyoro na akahamia Kyango (Buganda)

3
Nyamutura
Alifia Kyango (Buganda)

4
Lwekika I
Alifia Mayanja (Buganda)

5
Kagoro II
Alliingia Missenyi na kuwa Mwami wa kwanza wa Missenyi

6
Nyamutura II


7
Kagoro III
Hakuwa na mtoto wa kiume; kaka yake mdogo alirithi

8
Kyamukuma I
Kaka yake Kagoro III

9
Lwekika II
Mukama wa kwanza wa Missenyi
1870 – 1903
10
Suleimani Kakoko Wakara II

1913 – 1919
11
Paulo Nyamutura Lwamujongo I

1919 – 1955
12
Serapion N.L. Kyamukuma II

8 Feb 1955 – 22 Machi 2001

Kwa mujibu wa historia iliyotolewa, chimbuko lao ni Unyankole, Uganda. Maelezo zaidi:
Watawala wa Bunyoro walikuwa Wahima. Jamaa zao walikuwa wa ukoo wa Balebeki. Rumonge, mtawala mdogo wa Kihima huko Ankole alipoasi Bunyoro alifukuzwa. Nafasi yake ilichukuliwa na mtu wa ukoo wa Balabeki. Sehemu ya kusini ya Ankole mpakani mwa Mto Kagera ilikuwa Kibumbilo ambako mtawala mdogo wa Kihima, Kakoko, alitawala. Naye pia alikuwa wa ukoo wa Balebeki

Mwisho Kibumbilo ilikuwa sehemu ya Himaya ya Baganda mpaka ilipowekwa mipaka ya Wajerumani na Waingereza. Kwa hiyo historia ya utawala huu kwa Missenyi kabla ya matokeo haya haimo katika kitabu cha historia ya Buhaya.

Mwana ukoo wa Omukama wa Missenyi (kulia) akitoa maelezo ya historia mbele ya sehemu ambapo Omukama Serapion Kyamukuma alipokelea wageni wake.
Kabla ya kutawazwa mwaka 2011 Omukama Lwamujongo II alikuwa Dar es Salaam, ambako alikuwa anafanya kazi.

No comments: