Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, June 15, 2011

Leo katika historia ya Kombe la Dunia 2006: Poland, Trinidad & Tobago, na Paraguay zaaga mashindano


Poland, Trinidad & Tobago, na Paraguay ziliaga mashindano ya Kombe la Dunia.

Poland ilipoteza michezo yake yote miwili ya Kundi A, kwanza kwa Ecudaor (0-2), halafu kwa Ujerumani (0-1). Ingawa ilishinda mechi yake dhidi ya Costa Rica (2-1), haikutosha kuivusha na kuingia raundi ya pili. Ni ushindi wa Ecuador wa 3-0 dhidi ya Costa Rica uliyoivusha Ecuador, na kuiondoa Poland kwenye mashindano.

Trinidad & Tobago, katika ilipangwa na England, Sweden, na Paraguay katika Kundi B. Yenyewe ilitoka sare mechi moja tu na Sweden (0-0), na kupoteza mechi mbili. Tarehe ya leo, mwaka 2006, Trinidad & Tobago ililazwa 2-0 na England na kuyaaga mashindano, ikiwa ya mwisho kweye kundi lake.

Paraguay, ilishika nafasi ya pili toka mwisho kwenye kundi lake baada ya kufungwa 1-0 na Sweden, tarehe 15 Machi 2006, na timu ikapanda ndege kurudi Ascuncion.

Kwenye Kundi A Ujerumani na Ecuador ziliingia randi ya pili, wakati ni England na Sweden zilizoingia raundi ya pili toka Kundi B.

No comments: