Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, June 18, 2011

Tarehe za kupanda Mlima Kilimanjaro mwaka huu ni Septemba 20 hadi 27

Kila mwaka tangu mwaka 2008 nimekuwa napanda Mlima Kilimanjaro kuchangisha pesa za hisani. Mwaka 2008 nilipanda Mlima huo na raia wa Vietnam, Le Hu Dyuong. Mwaka 2009 nilipanda Kilimanjaro na Notburga Maskini, ambaye tulisoma pamoja Shinyanga Commercial Institute (Shycom) miaka iliyopita. Yeye alikuwa pamoja na mtangazaji maarufu wa Clouds FM, Gerald Hando.
Le akiwa kwenye bwawa lenye mamba, baada ya msafara wa kupanda Mlima Kilmanjaro mwaka 2008.
Mwaka jana nilipanda mlima na Jaffar Amin, mtoto wa kiongozi wa zamani wa Uganda, Idi Amin.
Jaffar Amin, akiwa amekaa mbele ya mahema yetu kwenye kambi ya Karanga iliyopo mita 3,963 juu ya usawa wa bahari wakati wa msafar wa mwaka jana wa kupanda Mlima Kilimanjaro.
Mwaka huu natarajia kupanda Mlima Kilimanjaro kuanzia tarehe 20 hadi 27 Septemba. Natarajia kupanda mlima pamoja na wafuatao. Ambao wamesema watajiunga na mimi mwaka huu ni pamoja na mwanablogu mwashuhuri Muhidini Issa Michuzi, mdau wa Utalii Aysha Boma, raia wa Uswisi Andrea Wobmann, mtengeneza filamu wa Marekani Jim Becket (amewahi kuongoza picha ya Mark Dacascos) pamoja na mpigapicha wake, na raia wa Uganda Barbara Allimadi. Kuna wengine ambao bado hawajathibitisha.

No comments: