Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, July 12, 2011

Siasa ya Tanzania: chama na sera zake, au mtu?


Kwenye picha ya hapa chini anaonekana diwani wa kata ya Muleba, Hassan Milanga wa Chama cha Wananchi (CUF), mwenye fulana nyekundu, akiteta jambo na wapiga kura wake wa mjini Muleba, ambao pia ni wafanyabiashara wa samaki. Milanga aliingia kwenye siasa mwaka 2000 na akachaguliwa kuwa diwani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM).
Kutokana na kile anachokieleza kuwa ‘mizengwe’ilizomzuwia kubaki CCM wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 alihamia CUF, na wapiga kura wakahama naye na kumchagua kwa mara ya pili kuwaongoza kama diwani wao.

Wapiga kura wakarudia tena kufanya hivyo hivyo mwaka 2010. Ni dhahiri kuwa kwa sehemu nyingi za Tanzania wapiga kura wanachagua mtu na siyo chama. Swali: Ina maana wagombea wanapoteza muda kunadi sera wakati wa kampeni?

No comments: