Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, July 15, 2011

Wageni wa Butiama: Dk. Thomas Molony


Mtafiti mwandamizi wa Kituo cha Masomo ya Afrika kilichopo Chuo Kikuu cha Edinburgh, Dk. Thomas Molony, yuko kijijini Butiama mwezi huu wa Julai akiandika kitabu juu ya muasisi wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (1922 – 1999).
Dk. Thomas Molony
Kitabu hicho kitahusu sehemu ya maisha ya Mwalimu kati ya mwaka 1922 alipozaliwa hadi mwaka 1952, baada tu ya kuhitimu masomo yake kwenye Chuo Kikuu cha Edinburgh na kabla hajajitupa kwenye harakati za kudai uhuru toka kwa Waingereza. 

Kwa kujiandaa na uandishi wa kitabu hiki, Dk. Molony amefanya utafiti nchini Uingereza na Tanzania na ni mara yake ya pili kutembelea Butiama. Anatarajia kitabu chake kitachapishwa kabla ya mwisho wa mwaka, kuwahi maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru tarehe 9 Desemba.

No comments: