Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, March 21, 2013

Mada yangu ya leo: Viongozi wakae maofisini na kupunguza uzinduzi

Kwa maoni yangu, viongozi wetu hawana muda wa kutosha kukaa kwenye ofisi zao na kufanya kazi ambayo walipa kodi wanatarajia zisimamiwe na viongozi wao. Sababu kubwa inayosababisha tatizo hili ni viongozi wetu kukubali mialiko ya uzinduzi wa kila jambo ambalo Watanzania wanaweza kubuni.

Na hapa sizungumzii viongozi wakuu tu wa nchi, nazungumzia viongozi wa ngazi zote kwa sababu nchini Tanzania imekuwa desturi sasa kwa kila jambo kuwa na uzinduzi rasmi, kuanzia kanda mpya ya kwaya mpaka kinywaji kipya.

Lakini ni dhahiri kuwa mifano inayopatikana kwa urahisi inawahusu viongozi wakuu wa nchi kwa kuwa habari zao zinaandikwa zaidi kuliko zile za viongozi wa ngazi za chini.

Angalia mifano ifuatayo ya Rais, Makamu wa Rais, na Waziri Mkuu, na utapata picha ya ukubwa wa tatizo hili:

Rais Jakaya Kikwete
Makamu wa Rais Dk. Mohamed Bilal
Waziri Mkuu Mizengo Pinda

Ni dhahiri kuwa kwa kila kiongozi kuna sehemu au shughuli fulani ambayo anapaswa kuhudhuria kwa sababu ya umuhimu wa shughuli yenyewe na nafasi yake katika uongozi, lakini ni dhahiri kuwa kuna shughuli nyingine nyingi ambazo hazina umuhimu kwa viongozi wetu kuhudhuria.

Kuna umuhimu kwa sheria kutumika kutamka shughuli rasmi ambazo viongozi wa ngazi ya Taifa wanapaswa kuhudhuria ili kupunguza mlolongo wa shughuli ambazo tunaoona zinazinduliwa na viongozi hawa. Hili likifanyika, litapunguza gharama kwa serikali na pia kuwapa muda mkubwa zaidi viongozi wetu kubaki kwenye sehemu zao za kazi na kusimamia vyema shughuli za serikali.

Kama nilivyosema awali, hapa nimetoa mifano ya viongozi wa kitaifa kwa sababu ndiyo mifano iliyo rahisi kuitoa. Lakini hili ni tatizo lililopo katika ngazi zote, kuanzia mawaziri mpaka watendaji wa vijiji.

Watanzania nao wabadilishe fikra kuwa haiwezekani kuchapa kazi bila kufanya uzinduzi.

No comments: