Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, March 9, 2013

Mwenyekiti wa ABETO atembelea Butiama

Moses Musana, mwenyekiti wa Always Be Tolerant Organisation (ABETO), azaki ya nchini Uganda, amefanya ziara kijijini Butiama hivi karibuni.

ABETO iliundwa mwaka 1966 ikiwa na madhumuni ya kuhimiza jamii katika bara la Afrika kutumia njia za amani kutatua migogoro, kuishi kwa amani, kudumisha uvumilivu, demokrasia, na utawala bora.
Mwenyekiti wa ABETO, Moses Musana (kushoto), akisalimiana na Mama Maria Nyerere wakati wa ziara aliyofanya kijijini Butiama hivi karibuni
Katika hafla iliyofanyika jijini Kampala tarehe 11 Agosti 2012, ABETO ilitoa tuzo ya amani kwa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo ilipokelewa na Mama Maria Nyerere.

Taarifa zinazohusiana na hizi:
http://muhunda.blogspot.com/2012/12/mkutano-wangu-na-jaffar-idi-amin.html
http://muhunda.blogspot.com/2011/07/wageni-wa-butiama-ujumbe-wa-veta.html
http://muhunda.blogspot.com/2010/09/wageni-toka-jkt-wamtembelea-mama-maria.html

No comments: