Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, March 9, 2013

Wahisani wachangia mabati 33 kwa ujenzi wa shule Kichalikani

Agnes Mambo anaarifu kuwa mabati 33 yamepokelewa hivi karibuni kuchangia ujenzi wa shule ya Msingi Kichalikani iliyopo Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.

Katika jitihada za kuchangia shule hiyo, mimi natarajia kukwea Mlima mwezi Juni 2013 kuchangisha pesa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huo. Msafara wangu ulipangwa mwezi huu lakini nimelazimika kuahirisha mpaka mwezi Juni.
****************************************
Na Agnes Mambo,MKINGA.
MKUU wa wilaya ya Rufiji mkoani Mwapwani, Nurdini Babu, na Mkurugenzi wa idara ya Teknolojia ya Habari IT, katika Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) la jijini Dar es salaam, Said Masimango, wametoa msaada wa bati 33 zenye thamani ya Shilingi 760,000/- katika shule ya Msingi Kichalikani wilayani Mkinga mkoani Tanga.
Jengo la Shule ya Msingi Kichalikani.
Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Rufiji mkoani Pwani mwenyekiti wa Tanga Village Support, Hassani Kibhondah, amesema kuwa lengo la kutoa msaada huo ni kusogeza huduma ya elimu karibu kutokana na wanafunzi wa eneo hilo kutembea umbali wa kilometa tatu kutoka Kichalikani hadi Shule ya Msingi Mongavyeru.

Mwenyekiti huyo amesema kuwa wadau hao wameguswa na kuchangia ujenzi wa shule hiyo ambayo ilianza kujengwa tangu mwaka 2009 kwa nguvu za wananchi wenyewe ambapo hadi sasa kuna vyumba viwili vya madarasa na ofisi mbili ,hivyo ameomba wapenda maendeleo kuguswa na suala hilo ili ujenzi uweze kukamilika.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa shule ya msingi Kichalikani, Jambia Ally Kubo, amesema kuwa watoto wanapata adha kubwa kutokana na maji ya bahari kujaa katika kisiwa hivyo kushindwa kuvuka ambapo wameiomba Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga kuchangia ujenzi wa shule hiyo.

Naye Mjumbe wa serikali ya kijiji cha Kichalikani, Amina Muhaji, awameshukuru wadau hao waliotoa vifaa hivyo ambapo amesema kuwa wanafunzi wanachapwa kutokana na kuchelewa kufika shule. Aliongeza kusema kuwa baadhi ya wanafunzi wanashindwa kuendelea na masomo wakihofia maisha yao kwa sababu ya kupita katika jangwa na kisiwa na kushindwa kuvuka.

Taarifa zinazohusiana na hizi:
http://muhunda.blogspot.com/2012/06/mwanzo-wa-msafara-wa-mlima-kilimanjaro.html

No comments: