Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, July 19, 2011

Takwimu: Viwango vya mfumuko wa bei kwa baadhi ya nchi Ulimwenguni


Kwa wachumi, kipimo kimojawapo cha hali ya uchumi ni kasi ya ongezeko la bei za bidhaa na huduma. Kwa ujumla, kasi kubwa ya ongezeko haileti manufaa kwa uchumi na kazi mojawapo muhimu ya Serikali yoyote ni kudhibiti ongezeko la bei kwa kupitia sera zake. Aidha, ongezeko la bei linapunguza uwezo wa wafanyakazi kumudu gharama za maisha na linaweza kuwa chachu ya migomo ya wafanyakazi na ukosefu wa amani kwenye nchi.

Sifa mojawapo ya Serikali ya Awamu ya Tatu ya Tanzania ya Rais Benjamin Mkapa ilikuwa mafanikio yake ya kudhibiti kasi ya mfumuko wa bei.

Zipo nchi kadhaa duniani ambazo takwimu zake zinaonyesha kuanguka kwa mfumuko wa bei. Maana yake, ni kuwa bei za bidhaa na huduma zinapungua badala ya kupanda. Hizi, kwa mujibu wa wavuti ya Wikipedia ni pamoja na Seychelles, Ireland, na Gabon.

Orodha kamili ya Wikipedia inapatikana hapa. Baadhi ya nchi zilizopo kwenye orodha hiyo na kasi ya ongezeko la mfumuko wa bei ni kama ifuatavyo:

Nafasi Duniani
Nchi
Kasi ya Mfumuko wa Bei (%)
1
Seychelles
-2.2
2
Ireland
-1.6
3
Gabon
-1.3
7
Japan
-0.7
24
Ujerumani
1.1
27
Senegal
1.2
34
Burkina Faso
1.4
34
Marekani
1.4
40
Canada
1.6
50
Cameroon
1.9
55
Umoja wa Falme za Imarati
2.2
84
Libya
3.0
92
Uingereza
3.3
121
Kenya
4.2
130
Afrika ya Kusini
4.5
140
China
5
142
Zimbabwe
5.03
166
Rwanda
6.4
179
Tanzania
7.2*

*Hizi ni takwimu za 2010

1 comment:

Anonymous said...

Kwa mfumuko huo wa bei maish bora ni ndoto.