Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, May 28, 2012

Maandalizi ya kupanda Mlima Kilimanjaro mwezi ujao

Kuna maandalizi mengi muhimu katika kujiandaa kupanda mlima Kilimanjaro. Suala moja muhimu sana ni kufanya mazoezi ya kutosha kabla ya kwenda mlimani, mazoezi yanayopaswa kufanywa kwa muda wa miezi mitatu kabla ya msafara.
Kuna viatu maalum kwa ajili ya kukwea milima mirefu. Wataalamu wanashauri kuwa viatu hivyo vitumike kwanza kabla ya kuanza msafara na vivaliwe kwa muda ili mtumiaji avizowee. Kutumia viatu kabla ya msafara kunasaidia pia kufahamu iwapo havibani sana na vinamtosha mtumiaji barabara.
Nikiwa najiandaa kueleka tena Mlima Kilimanjaro mwezi ujao kwa mara ya tano nikiwa na kundi la wageni toka Marekani ambao pamoja nao tunachangisha pesa kwa ajili ya ujenzi wa maktaba ya shule ya Sekondari ya Nyegina iliyopo jirani na Musoma, nimeanza kutumia viatu hivi juma moja kabla ya kuanza msafara wa kupanda Mlima Kilimanjaro. Viatu hivi nimeshavitumia mara kadhaa kwenye misafara iliyopita ya Mlima Kilimanjaro.

No comments: