Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, December 21, 2012

Ushauri wa bure kuhusu uendeshaji wa gari

Hii makala ni tafsiri ya makala yangu ya Kiingereza ambayo ilichapishwa tarehe 1 Mei 2005 kwenye makala zangu "Letter from Butiama" nilizoandika kwenye gazeti la Daily News kati ya mwaka 2005 na 20011.
*************************************************
Ikiwa habari za siasa na hususan mkutano wa wiki ijayo wa uteuzi wa mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi kushamiri kwenye kinywa cha kila mtu mimi nageukia mada ambayo haihusiani kabisa na siasa, uendeshaji gari. Huu ni ushauri ambao unaweza kuutumia kukuwezesha kuendesha gari kwa usalama zaidi na kukuepusha na hali za kushtukiza, hasa pale unapokuwa kwenye masafa marefu.

Huu siyo ushauri wa juu juu kama ule wa kukutaka ukague maji ya rejeta kabla hujaanza safari. Ni ushauri ambao pengine hutafundishwa kwenye vyuo vya udereva. Huu ushauri unatolewa na mtu ambaye ameendesha gari kwa karibia miaka 25 akiwa na ajali moja tu ndogo.

Bado sijakutana na dereva ambaye anakiri kuwa yeye ni dereva asiye wa viwango. Kwa hiyo kanuni ya kwanza ya uendeshaji gari ni: kabla hata hujawasha gari ni muhimu kujiamini; usipojiamini hakuna mtu mwingine atakayekuamini. Jichukulie kama ni mwendeshaji bora kuliko wote duniani; kile unachopungukiwa utakipata kutokana na uzoefu. Lakini usichukulie huu ushauri kwa maana yake halisi, yaani neno kwa neno kwa sababu pamoja na kuwa unajiamini bado utahitaji mafunzo ya msingi ya udereva, pamoja na kuwepo ukweli kuwa kuna watu ambao wameweza kujifunza kuendesha gari baada ya kupata leseni zao.

Kanuni ya pili ni usitoe lifti kwa watu usiowafahamu, hasa wanaume. Kuna wanaume wengi zaidi wenye makusudio ya kutenda uhalifu kuliko wanawake wenye tabia za aina hiyo. Matokeo ya tafiti ulimwenguni yanaonyesha kuwa kuna wanaume wengi zaidi wanaokutwa na hatia za jinai zaidi ya wanawake. Kwa Uingereza kwa mwaka 1984 idadi ilikuwa 86%. Kama moyo wako unakutuma kuwasaidia wenye shida nashauri utoe lifti kwa wanawake tu, lakini kuwa mwangalifu na warembo. Mara nyingine, nyuma ya mwanamke mrembo anayeomba lifti hujificha mwanaume mwenye sura mbaya mwenye nia mbaya.

Ni maoni yangu kuwa mtu ambaye ni salama kabisa kumsaidia ni mwanamke mzee. Au bora zaidi, mwanamke mwenye watoto. Yumkini kuwa hata mwanamke mwenye kusudio la kutenda kosa la jinai atawaacha watoto wake nyumbani kabla ya kujaribu kuteka nyara gari.


Kanuni ya tatu: epuka kusimamisha gari kusaidia mtu ambaye anaonekana kama amejeruhiwa na umemkuta kalala barabarani. Mwezi Novemba mwaka jana, nikiwa safarini kutoka Mwanza kwenda Dodoma, nilikuta kizuizi barabarani usiku na mtu mmoja ambaye alikuwa amevaa kiraia alijitokeza akiwa na silaha ya kijeshi. Nilihisi kuwa na polisi kwa sababu hakuelekeza silaha dhidi yangu kudai nimpe pesa. Kabla sijaondoka alinitahadharisha kuwa kilomita 40 zilizobaki kuelekea Dodoma lilikuwa ni eneo la hatari na akaniuliza, "Unafahamu kanuni za kuendesha gari usiku?"

Nilimuuliza: "Kwa mfano?"
Akasema: "Kwa mfano, ukikuta mtu kalala barabarani utafanya nini?
Nikamwambia: "Nitamkwepa halafu nitarudi kesho asubuhi kuangalia kama bado yuko pale."
Akaniambia: "Endelea na safari. Unafahamu kanuni za uendeshaji usiku."

Kanuni ya nne: Endesha kwa kasi kubwa unayataka ukiwa mwenyewe. Unayo haki ya kusitisha maisha yako kama hiyo inakupendezesha lakini pindi unapokuwa na abiria kwenye gari yako basi onyesha staha kidogo kwa hulka ya kila mwanadamu ya kutaka kuishi milele. Nilivunja hiyo kanuni mara moja na sikujuta kufanya hivyo. Niliendesha gari toka Songea hadi Dar es Salaam nikiwa na abiria kwa mwendo wa kasi wakati wa ile safari. Tulipofika nusu ya safari tulifika tulisimama kwenye milima ya Kitonga kwa dakika chache kununua mahindi ya kuchoma njiani. Dakika 20 kabla ya kufika hapo tulikuwa tumepita mabasi mawili ya abiria ambayo yalipofika eneo lile lile (wakati sisi tulikuwa tumeshaondoka) yalivamiwa na majambazi yenye silaha ambayo yalimjeruhi kwa risasi aliyefika kwenye eneo wakati tukio la utekaji linaendelea.

Siku iliyofuata tuliposikia habari za lile tukio la ujambazi tuliafikiana kuwa jambo lililonisukuma niendeshe gari kwa kasi kubwa lilituokoa kuwepo kwenye shambulio lile la ujambazi.


Ni bora pengine kuongezea kuwa, wakati mwingine, uendeshaji wa kasi unaweza kutumika kuepukana na hali ya hatari (nakumbuka hii kanuni kutoka kwenye mafunzo yangu ya udereva miaka 25 iliyopita).

No comments: