Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, December 5, 2012

Mtanzania Mariagoreth Ndangio afariki Uingereza, mwili wasafirishwa nyumbani kwa mazishi

Jana, tarehe 4 Desemba 2012, muda wa saa tano Watanzania waishio Luton Uingereza, ndugu na marafiki kwa ujumla walijumuika katika kanisa la Kikatoliki la Holy Ghost Westbourne, Luton, Uingereza, katika ibada ya kumuaga MariaGoreth Ndangio tayari kwa safari ya mazishi kuelekea nyumbani Tanzania.
Marehemu Mariagoreth Ndangio
Katika ibada hiyo mama mzazi wa marehemu aliwashukuru watu wote waliojitoa kwa kila hali wakati wa kumuuguza mwanae mpaka mauti ilipomkuta. Pia kaka wa marehemu alisoma historia fupi ya marehemu na kueleza upendo na ushirikiano aliokuwa nao na watu wote.

Mwili wa marehemu unatarajiwa umesafirishwa leo Jumatano kuelekea Tanzania kwa ajili ya mazishi.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Luton ( Luton Tanzanian Community ) Bw. John Mbwete kwa niaba ya familia ya marehemu na Jumuiya ametoa shukurani kubwa kwa watu wote waliojitoa kwa hali na mali, Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza na Tanzania Association kwa ushirikiano waliotoa katika kufanikisha safari ya mwisho ya Mariagoreth kuelekea Tanzania.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa, sifa na utukufu kwa Mwenyezi Mungu.
Shukrani.
*******************************
Taarifa imetolewa na:
Abraham Sangiwa
Katibu – Luton Tanzanian Community ( TLC )

No comments: