Kuna maandalizi mengi muhimu katika kujiandaa kupanda mlima Kilimanjaro. Suala moja muhimu sana ni kufanya mazoezi ya kutosha kabla ya kwenda mlimani, mazoezi yanayopaswa kufanywa kwa muda wa miezi mitatu kabla ya msafara.
Kuna viatu maalum kwa ajili ya kukwea milima mirefu. Wataalamu wanashauri kuwa viatu hivyo vitumike kwanza kabla ya kuanza msafara na vivaliwe kwa muda ili mtumiaji avizowee. Kutumia viatu kabla ya msafara kunasaidia pia kufahamu iwapo havibani sana na vinamtosha mtumiaji barabara.
Nikiwa najiandaa kueleka tena Mlima Kilimanjaro mwezi ujao kwa mara ya tano nikiwa na kundi la wageni toka Marekani ambao pamoja nao tunachangisha pesa kwa ajili ya ujenzi wa maktaba ya shule ya Sekondari ya Nyegina iliyopo jirani na Musoma, nimeanza kutumia viatu hivi juma moja kabla ya kuanza msafara wa kupanda Mlima Kilimanjaro. Viatu hivi nimeshavitumia mara kadhaa kwenye misafara iliyopita ya Mlima Kilimanjaro.
Monday, May 28, 2012
Saturday, May 19, 2012
Dimpoz kuzindua 'single' yake mpya Bilicanas Dar Jumapili 20 Mei 2012
Taarifa toka Mroki Mroki zinasema kuwa msanii Omy Dimpoz atazindua 'single' yake mpya leo kwenye Klabu ya Bilicanasa ya Jijini Dar es Salaam. Picha na habari kwa hisani ya Mroki Mroki wa Digital Company & FK Blog.
BAADA ya kutamba na wimbo wake wa Nai Nai, msanii anaekuja juu kwa kasi na mshindi wa Tuzo mbili za Kili Music Award 2012, Omy Dimpoz, anataraji kuzindua 'single' yake mpya ya Baadae katika ukumbi wa Club Bilicanas jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mtandao huu wa Kijamii, meneja wa msanii huyo, Mbaruku Issa ‘Mubenga’ alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika na show itakuwa ya uhakika na ya kuvutia.
Mubenga amesema Ommy Dimpoz anataraji kuzindua wimbo huo alioufanyiwa kazi na mwandaaji wa muziki Man Water huku akkimba pamoja na mwanadada Angel.
Aidha Mubenga amesema Dimpoz atasindikizwa na wakali wa Bongo Fleva, Diamond, Ben Pol pamoja na msanii Alawi Jr pamoja na Ma DJ wakali wa Bongo kutoka kundi la Super Deejayz.
Tayari Dimpoz ameshaanza kuwasikilizisha wimbo huo baadhi ya mashabiki wake wa mikoa ya Mwanza na Moshi wakati wa Ziara ya Wakali wa Kili Music Awartd 2012 inayoendelea ambapo leo atakuwa Mbeya chini ya udhamini wa bia ya Kilimanjaro.
“Wimbo ni mkali na mashabiki wanaukubali vilivyo na tunaomba mashabiki wa Bongo Fleva make tayari kwa singo hiyo mpya itakayoanza sasa kuchezwa katika vituo vya redio na kumbi za burudani nchini kote baada ya uzinduzi huo,” alisema Mubenga.
Mubenga amewataka wakazi wa Jiji la Dar es Salaam ambao ni mashabiki na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono Dimpoz katika uzinduzi huo wa aina yake katika Klabu ya Bilicanas katikati ya jiji la Dar es Salaam Jumapili.
BAADA ya kutamba na wimbo wake wa Nai Nai, msanii anaekuja juu kwa kasi na mshindi wa Tuzo mbili za Kili Music Award 2012, Omy Dimpoz, anataraji kuzindua 'single' yake mpya ya Baadae katika ukumbi wa Club Bilicanas jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mtandao huu wa Kijamii, meneja wa msanii huyo, Mbaruku Issa ‘Mubenga’ alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika na show itakuwa ya uhakika na ya kuvutia.
Mubenga amesema Ommy Dimpoz anataraji kuzindua wimbo huo alioufanyiwa kazi na mwandaaji wa muziki Man Water huku akkimba pamoja na mwanadada Angel.
Aidha Mubenga amesema Dimpoz atasindikizwa na wakali wa Bongo Fleva, Diamond, Ben Pol pamoja na msanii Alawi Jr pamoja na Ma DJ wakali wa Bongo kutoka kundi la Super Deejayz.
Tayari Dimpoz ameshaanza kuwasikilizisha wimbo huo baadhi ya mashabiki wake wa mikoa ya Mwanza na Moshi wakati wa Ziara ya Wakali wa Kili Music Awartd 2012 inayoendelea ambapo leo atakuwa Mbeya chini ya udhamini wa bia ya Kilimanjaro.
“Wimbo ni mkali na mashabiki wanaukubali vilivyo na tunaomba mashabiki wa Bongo Fleva make tayari kwa singo hiyo mpya itakayoanza sasa kuchezwa katika vituo vya redio na kumbi za burudani nchini kote baada ya uzinduzi huo,” alisema Mubenga.
Mubenga amewataka wakazi wa Jiji la Dar es Salaam ambao ni mashabiki na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono Dimpoz katika uzinduzi huo wa aina yake katika Klabu ya Bilicanas katikati ya jiji la Dar es Salaam Jumapili.
Wednesday, May 16, 2012
HakiElimu yatoa zawadi ya vitabu kwa maktaba ya Mwalimu J.K. Nyerere
Asasi ya HakiElimu hivi karibuni imetoa zawadi ya vitabu kadhaa kwa maktaba ya Mwalimu J.K. Nyerere iliyopo Butiama.
Maktaba ya Mwalimu J.K. Nyerere inatunza mkusanyiko wa vitabu binafsi zaidi ya 8,000 vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambavyo alivikusanya katika kipindi chote cha maisha yake, na ipo kwenye makazi yake yaliyopo kijijini Butiama.
Vitabu zaidi ya 50 vilivyotolewa na HakiElimu vitatunzwa kwenye maktaba hiyo, ambayo ni kivutio kimojawapo kati ya vivutio kya wageni wanaotembelea kijiji cha Butiama, sehemu alipozaliwa Mwalimu Nyerere tarehe 13 Aprili 1922, na ambapo alizikwa tarehe 23 Oktoba 1999.
Maktaba ya Mwalimu J.K. Nyerere inatunza mkusanyiko wa vitabu binafsi zaidi ya 8,000 vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambavyo alivikusanya katika kipindi chote cha maisha yake, na ipo kwenye makazi yake yaliyopo kijijini Butiama.
![]() |
Zawadi ya vitabu iliyotolewa na HakiElimu katika maktaba ya Mwalimu J.K. Nyerere, kijijini Butiama. |
Sunday, May 13, 2012
Timu ya waTanzania DMV yatoka sare na Ethiopia B
Timu ya waTanzania DMV imetoka sare, bila kufungana, na timu ya Ethiopia B katika mchezo uliochezwa jana huko Burtonsville, Maryland, nchini Marekani katika ligi ya Diaspora World Cup.
Saturday, May 12, 2012
Timu ya Tanzania DMV kuchuana na Ethiopia (B) leo
Katika mchezo wa ligi ya 2011 Diaspora World Cup unaoendelea katika viwanja
vya Hyattsville na Germantown, jijini Maryland nchini Marekani, timu ya Tanzania
DMV itachuana vikali na timu ya Ethiopia leo hii Jumamosi May 12, 2012 saa 6:00 mchana katika kiwanja cha Greencastle, kilichopo Burtonsville,
Maryland.

Kundi (B) Timu ya wa Ethiopia katika mchezo wa
awali walifungwa mabao 3-0 na timu ya Malawi ndani ya uwanja cha Greencastle,
Burtonsville, Maryland. Leo Ethiopia watajiandaa vikali ili kutaka kurudisha nguvu
zao kwa mchezo waliopoteza dhidi ya timu hiyo ya Malawi, ambayo leo itapambana na Armenia saa 7:00 mchana.
Katika mechi ya awali Armenia waliwabamiza Nigeria bao 4-1.
Tanzania DMV katika mchezo wa
kwanza siku ya Jumapili 29 April 2012 walifanikiwa kuwabamiza Ghana
mabao 3-2 ndani ya uwanja wa SoccerPlex Stadium uliyopo Ager Road Hyattsville
Maryland.
Kama kawaida yao timu ya Tanzania DMV inawaomba Watanzania wote ushirikiano wenu ili kuipa changamoto timu ya Watanzania DMV. Mnaombwa pia kufika mapema saa 5:00 kuzowea mazingira kabla ya mchezo huo kuanza.
Sehemu ya mchezo utakaochezwa leo hii ni Fairland Field 3928 Greencastle Rd. Burtonsville, Maryland 20866 Habari na http://swahilivilla.
Habari na picha kutoka http://swahilivilla.
Wednesday, May 9, 2012
Bondia Selemani Kidunda afuzu kushiriki michezo ya Olimpiki ya London
Pichani, mwenyekiti wa chama cha ngumi za ridhaa Tanzania, Michael Changarawe, kushoto, akimpongeza bondia Selemani Kidunda kwa kufuzu kushiriki michezo ya Olimpiki ya London Uingereza akiiwakilisha Tanzania.
Michezo ya Olimpiki itachezwa jijini London kuanzia tarehe 27 Julai hadi 12 Agosti, 2012.
Picha na habari kwa hisani ya superboxingcoach.
Michezo ya Olimpiki itachezwa jijini London kuanzia tarehe 27 Julai hadi 12 Agosti, 2012.
Picha na habari kwa hisani ya superboxingcoach.
Lugha yetu Kiswahili
Kwa Kiswahili sanifu, kofia ya rangi nyekundu anayovaa Mhe. Nimrod Mkono, mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, inaitwa tarabushi. Aidha, huitwa pia tarbushi.
Asili ya tarabushi ni eneo la Ugiriki ya kale lakini ni kofia ambayo huvaliwa sana na Waislamu wa eneo la mashariki la Bahari ya Mediterenia. Mpaka mwaka 1925 kofia hii ilikuwa sehemu ya vazi rasmi nchini Uturuki.
Bango la barabarani lenye picha ya Mhe. Nimrod Mkono akiwa amevaa tarabushi, akiwa pamoja na Rais Jakaya Kikwete, kulia. |
Tuesday, May 8, 2012
Ngowi kusimamia pambano la ubingwa wa IBF nchini Ghana
|
Thursday, May 3, 2012
Harusi za siku hizi
Bwana Harusi akitambulisha familia yake katika mojawapo ya harusi za miaka ya hivi karibuni. |
Kwenye harusi za zamani maharusi walikaa kimya na kujionyesha kama watu wataratibu sana, hata kama ukweli ulikuwa tofauti na taswira iliyoonekana. Leo hii kwenye harusi maharusi huonyesha hisia zao waziwazi na wanacheza muziki katika kila hatua ya sherehe: kuanzia kupokea zawadi toka kwa wageni, mpaka wakati wa kusogelea meza wakati wa kukata keki ya harusi.
Subscribe to:
Posts (Atom)