Makelele ni mojawapo ya kero za miji ambayo sehemu kama Butiama haikuwa nayo mpaka hivi karibuni. Butiama haikuwa na huduma ya basi linalosafiri moja kwa moja kwenda Mwanza na hapo awali wasafiri walilazimika kusafiri mpaka njia kuu iendayo Mwanza, sehemu iitwayo Nyamisisi, au kuanzia safari Musoma. Miaka michache iliyopita huduma ya basi la moja kwa moja kutoka Butiama hadi Mwanza ilianzishwa na kuleta kero ninazozungumzia.
![]() |
Basi la kuelekea Mwanza kwenye stendi ya Butiama. |
Sijaelewa mantiki ya kupiga hizo honi ingawa naamini zinakusudiwa kuwaamsha abiria wanaosafiri.Lakini ni vigumu kuelewa utaratibu wa abiria anaekusudia kwenda Mwanza kutegemea kuamshwa na honi ya basi.