Taasisi ya Masomo ya Afrika ya Chuo Kikuu cha Georgia inatoa mafunzo ya lugha ya Kiswahili kwa njia ya mtandao.
Maelezo yaliyopo kwenye tovuti inayoitwa Kiswahili kwa Komputa yanaonyesha kuwa kozi hiyo ya Kiswahili inaendeshwa kwa kipindi cha miaka mitatu na inaelekea kuwa hufundishwa darasani pamoja na nyongeza ya masomo yaliyopo kwenye tovuti hiyo.
Mbali na kuwa Kiswahili sahihi ni "kompyuta" na siyo "komputa" na kuwa baadhi ya matamshi yaliyorekodiwa kwa njia ya sauti yanatofautiana na matamshi niliyozowea kusikia (mfano "redio" inatamkwa "radio"), tovuti hiyo bado inaweza kuwa ya manufaa makubwa na inaweza kumsaidia mwanafunzi yoyote wa lugha ya Kiswahili ambaye anafahamu vyema Kiingereza na anaweza kujifunza mwenyewe kutokana na maelezo yaliyopo.
Anwani ya tovuti hii hapa: http://www.africa.uga.edu/Kiswahili/doe/index.html
Kila mwaka wa masomo una sura sita, na kozi inakamilika kwa sura 18. Mwisho wa kila sura mwanafunzi anapaswa kufanya mtihani ambao unaweza kutumwa kwa njia ya mtandao kwa mwalimu kwa masahihisho.
Taarifa zinazohusiana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2013/02/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2013/01/lugha-yetu-kiswahili.html
Sunday, April 14, 2013
Tathmini ya muziki wa Tanzania mwaka 2012 (sehemu ya nne kati ya nne)
Katika makala hii nitakayoitoa katika sehemu nne, mwanamuziki mashuhuri John Kitime, anafanya tathmini ya hali ya muziki Tanzania mwaka 2012.
Ikiwa kulikuwa na mchango wa serikali katika muziki, basi ulikuwa mdogo au ulikuwa ni kwa shughuli maalumu lakini si kwa kutengeneza mazingira ya kuwezesha unafuu kwa wanamuziki kwa ujumla. Idara ya Utamaduni imeendelea kupata bajeti ndogo ambayo imefanya Baraza La Sanaa La Taifa kuendelea kubaki Dar es Salaam tu, likibangaiza kuweko kwa kutegemea kutoa vibali mbalimbali kwa wasanii, na nguvu zake kuonekana Dar es Salaam tu. Na kwa kuwa hakuna Maafisa Utamaduni Mkoa, na Maafisa Utamaduni Wilaya na Manispaa wako chini ya serikali za mitaa hivyo kuwa wizara tofauti na Waziri wa Utamaduni, nguvu za serikali katika utamaduni ni 0.
******************************************
Tathmini ya muziki wa Tanzania mwaka 2012
makala ya John Kitime
(Sehemu ya nne kati ya sehemu nne)
Ikiwa kulikuwa na mchango wa serikali katika muziki, basi ulikuwa mdogo au ulikuwa ni kwa shughuli maalumu lakini si kwa kutengeneza mazingira ya kuwezesha unafuu kwa wanamuziki kwa ujumla. Idara ya Utamaduni imeendelea kupata bajeti ndogo ambayo imefanya Baraza La Sanaa La Taifa kuendelea kubaki Dar es Salaam tu, likibangaiza kuweko kwa kutegemea kutoa vibali mbalimbali kwa wasanii, na nguvu zake kuonekana Dar es Salaam tu. Na kwa kuwa hakuna Maafisa Utamaduni Mkoa, na Maafisa Utamaduni Wilaya na Manispaa wako chini ya serikali za mitaa hivyo kuwa wizara tofauti na Waziri wa Utamaduni, nguvu za serikali katika utamaduni ni 0.
COSOTA,
chombo ambacho shughuli yake ilikuwa ni kulinda hakimiliki za wasanii na
ambacho kilikuwa chini ya wasanii, kwa kinyemela kabisa kimerudishwa katika
mikono ya serikali, lakini bado kinakusanya mirabaha 'kwa niaba ya wasanii'
huku kukiwa na bodi isiyo na uwakilishi wa wasanii kuanzia 2007. Swali:
utakusanyaje pesa kwa niaba yangu lakini huniruhusu kujua ni kiasi gani
umekusanya, unazitumiaje na ukiulizwa unakuwa mkali!!!!!!? Kuna wasanii
wamekuwa wakidai kurudishiwa COSOTA, ushauri wangu wasanii wakae
wajipange na kuelewa vizuri sheria ya Hakimiliki kabla ya kujitwishwa
zigo hilo la miba.
Katika
miezi sita ya mwisho ya 2012 kumejitokeza spidi kali ya Mamlaka ya Ukusanyaji wa
Mapato kutengeneza mazingira ya kukusanya mapato kutokana na mauzo ya kazi za
muziki na filamu. Kimsingi kulipa kodi ni wajibu wa kila mwananchi na wasanii
ni wananchi pia, lakini taratibu zake ndiyo zinanipa utata, hasa pale ambapo kwa
muda mrefu imekuwa ikitangazwa kuwa njia hii itasaidia wasanii kwa kupunguza
kuibiwa.
Sentensi
hii inaonyesha wazi anayeiongelea au hajui mfumo wa biashara ya kazi muziki,
au kwa makusudi anapotosha ili kuficha kitu. Wasanii wengi huwa wamekwishalipwa
kwa kazi ambazo zimesambaa na ziko barabarani zinaibiwa, wanaoibiwa ni
wasambazaji. Hivyo kulinda kazi hizo unamlinda msambazaji si msanii. Pia kuanza
kukusanya kodi kwa kazi hizi kumepewa jina ‘kurasimishwa kwa kazi ya usanii’.
Kuna mabilioni wasanii
wanatakiwa walipwe na watumiaji wa kazi za sanaa, kama redio na TV, mapromota,
waajiri na kadhalika lakini hakuna anaeliongelea hilo wala hakuna anaetamka
takwimu hizo. Kuna kazi ya kurudisha mitaala ya masomo ya sanaa mashuleni,
kurudisha vyuo vya walimu wa sanaa, kurudisha maafisa utamaduni kuwa chini ya
Wizara ya Utamaduni kuwawezesha kufanya kazi zao kadiri ya Sera ya Utamaduni, na
mengine mengi ya aina hiyo ndiyo ningeona kurasimisha kazi za sanaa. Lakini
kukusanya kodi tu kwa kazi ambazo hata hivyo mikataba yake mingi inautata na
kuita urasimishaji si sahihi.
Katika
nchi nyingi critics au watu ninaoweza
kuwaita Kiswahili wakosoaji, huwa ni muhimu katika maendeleo ya sanaa. Watu
hawa hupata heshima kutokana na kuweza kuangalia mapungufu katika kazi za sanaa
na kuyasema, jambo ambalo hupelekea wasanii kujirekibisha na kutengeneza kazi
bora zaidi. Hapa kwetu kutoa ushauri ni kutafuta matusi, toka kwa wasanii wenye
kazi husika, vyombo vya habari na hata sehemu ya jamii. Umefika muda wahusika
kuchukua uchambuzi kama changamoto za kuboresha kazi.
Niliyoyataja
hapa yote yako wazi. Ninachotegemea ni kuona 2013 hatua zinaanza kupigwa
kurekebisha ili wanamuziki wa nchi hii nao wapate nafasi sawa na wengine wa
nchi nyingine.
John
Kitime
31.12.2012
Sinza,
Dar es Salaam
Taarifa zinazohusiana na hii:
Friday, March 22, 2013
Tathmini ya muziki wa Tanzania mwaka 2012 (sehemu ya tatu kati ya nne)
Katika makala hii nitakayoitoa katika sehemu nne, mwanamuziki mashuhuri John Kitime, anafanya tathmini ya hali ya muziki Tanzania mwaka 2012.
******************************************
Tathmini ya muziki wa Tanzania mwaka 2012
makala ya John Kitime
(Sehemu ya tatu kati ya sehemu nne)
Tasnia
ya muziki wa Tanzania katika tafiti mojawapo umeitwa ‘the radio-driven contemporary music industry’. Kwa maneno rahisi,
tasnia ambayo imekuwa inaendeshwa na redio. Redio zimekuwa na uwezo wa
kumpandisha na kumshusha mwanamuziki, kumtafutia soko, kumzibia soko na
kadhalika. Hali hii ikisindikizwa na rushwa ambayo imetapakaa katika jamii
yetu, unapata picha kuwa kungeweza kukawa na sura bora au tofauti ya muziki
hali isingekuwa ilivyo.
Kuna
ripoti za watu kutoa hongo nyimbo za wenzao zisipigwe, hongo ili nyimbo
zipigwe, visasi vya kuzuia nyimbo zisipigwe na kadhalika. Na katika jamii
ambayo imekuwa na kawaida ya kutegemea vyombo vya habari kujua muziki gani mpya
na mzuri, uwanja huu si uwanja ulio tambarare hata kidogo. Bahati mbaya
inaonekana wenye vyombo hivi wako mbali na ukweli unaoendelea katika vyombo
vyao au kwa kutokujua au kupuuza.
Janga
hili limevikumba hata vyombo ambavyo vinaendeshwa na taasisi za dini.
Wanamuziki wa muziki wa injili nao pia wanalia kudaiwa rushwa na watangazaji wa
radio za injili!. Nakumbuka siku
niliyopata nafasi kuongea na kiongozi mmoja wa dini ambaye kanisa lake
linaendesha kituo cha redio, nilipata mshangao baada ya mkuu huyo, kuanza
kutetea watangazaji wake badala ya kuamua kufanya uchunguzi wa tuhuma.
Umefika
muda wa redio kuanza kujigawa kimuziki. Ni kichekesho mji kuwa na vituo vya redio
30 halafu vyote vinapiga aina hiyohiyo ya muziki, wakati kuna aina mbalimbali
za watu. Ajabu ni kuwa wenye redio wanajua kuwa katika nchi nyingine unaweza
kukuta redio iliyoamua kupiga aina fulani tu ya muziki, Jazz Radio, Country
music Radio, Classic Music Radio, lakini hilo limekuwa gumu kwao kutekeleza
hapa. Kuwe na utofauti, wasikilizaji tuko wa aina tofauti.
Vyombo
vya habari vijitahidi kupata wataalamu husika wa aina tofauti za muziki, muziki
unaviingizia vyombo hivyo mabilioni ya fedha, vyombo vya habari viupe heshima
yake. Bila muziki hakuna redio.
Magazeti
yamekuwa mstari wa mbele katika kutangaza aina mbalimbali za wasanii na sanaa.
Pamoja na hongera kwa kazi nzuri lakini bado kuna nafasi kubwa ipo tupu, hakuna
wataalamu wa uandishi wa habari za muziki. Hivyo habari nyingi za muziki
zinaandikwa na waandishi kama wapenzi wa muziki na si wataalam wa uandishi wa
muziki, jambo ambalo liko tofauti na uandishi wa michezo, kwa mfano soka.
Unaweza ukasoma habari ya soka ambapo mwandish atakueleza nafasi za wachezaji,
kama ni faulo, ni nini kilisababisha, na kama ni goli lilikuwa ni la kichwa au
kona au penalty. Hili haliko katika muziki. Utaambiwa tu bendi ilipagawisha, au
msanii fulani ateka nyoyo za wapenzi, na maelezo ya juu juu kama yale.
Kunahitajika
kuanzishwa mafunzo ya elimu ya uandishi wa kazi za sanaa. Hili litapunguza hata
vurugu kama zilizotawala mwaka huu za wapiga picha kufikia hata kulala
chini ili tu wapate picha ya nguo za ndani za msanii na hayo ndio kuwa maelezo
makuu ya onyesho zima la muziki.
(itaendelea)
Taarifa zinazohusiana na hii:
Thursday, March 21, 2013
Mada yangu ya leo: Viongozi wakae maofisini na kupunguza uzinduzi
Kwa maoni yangu, viongozi wetu hawana muda wa kutosha kukaa kwenye ofisi zao na kufanya kazi ambayo walipa kodi wanatarajia zisimamiwe na viongozi wao. Sababu kubwa inayosababisha tatizo hili ni viongozi wetu kukubali mialiko ya uzinduzi wa kila jambo ambalo Watanzania wanaweza kubuni.
Na hapa sizungumzii viongozi wakuu tu wa nchi, nazungumzia viongozi wa ngazi zote kwa sababu nchini Tanzania imekuwa desturi sasa kwa kila jambo kuwa na uzinduzi rasmi, kuanzia kanda mpya ya kwaya mpaka kinywaji kipya.
Lakini ni dhahiri kuwa mifano inayopatikana kwa urahisi inawahusu viongozi wakuu wa nchi kwa kuwa habari zao zinaandikwa zaidi kuliko zile za viongozi wa ngazi za chini.
Angalia mifano ifuatayo ya Rais, Makamu wa Rais, na Waziri Mkuu, na utapata picha ya ukubwa wa tatizo hili:
Rais Jakaya Kikwete
Makamu wa Rais Dk. Mohamed Bilal
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Ni dhahiri kuwa kwa kila kiongozi kuna sehemu au shughuli fulani ambayo anapaswa kuhudhuria kwa sababu ya umuhimu wa shughuli yenyewe na nafasi yake katika uongozi, lakini ni dhahiri kuwa kuna shughuli nyingine nyingi ambazo hazina umuhimu kwa viongozi wetu kuhudhuria.
Kuna umuhimu kwa sheria kutumika kutamka shughuli rasmi ambazo viongozi wa ngazi ya Taifa wanapaswa kuhudhuria ili kupunguza mlolongo wa shughuli ambazo tunaoona zinazinduliwa na viongozi hawa. Hili likifanyika, litapunguza gharama kwa serikali na pia kuwapa muda mkubwa zaidi viongozi wetu kubaki kwenye sehemu zao za kazi na kusimamia vyema shughuli za serikali.
Kama nilivyosema awali, hapa nimetoa mifano ya viongozi wa kitaifa kwa sababu ndiyo mifano iliyo rahisi kuitoa. Lakini hili ni tatizo lililopo katika ngazi zote, kuanzia mawaziri mpaka watendaji wa vijiji.
Watanzania nao wabadilishe fikra kuwa haiwezekani kuchapa kazi bila kufanya uzinduzi.
Na hapa sizungumzii viongozi wakuu tu wa nchi, nazungumzia viongozi wa ngazi zote kwa sababu nchini Tanzania imekuwa desturi sasa kwa kila jambo kuwa na uzinduzi rasmi, kuanzia kanda mpya ya kwaya mpaka kinywaji kipya.
Lakini ni dhahiri kuwa mifano inayopatikana kwa urahisi inawahusu viongozi wakuu wa nchi kwa kuwa habari zao zinaandikwa zaidi kuliko zile za viongozi wa ngazi za chini.
Angalia mifano ifuatayo ya Rais, Makamu wa Rais, na Waziri Mkuu, na utapata picha ya ukubwa wa tatizo hili:
Rais Jakaya Kikwete
Makamu wa Rais Dk. Mohamed Bilal
Waziri Mkuu Mizengo Pinda
Ni dhahiri kuwa kwa kila kiongozi kuna sehemu au shughuli fulani ambayo anapaswa kuhudhuria kwa sababu ya umuhimu wa shughuli yenyewe na nafasi yake katika uongozi, lakini ni dhahiri kuwa kuna shughuli nyingine nyingi ambazo hazina umuhimu kwa viongozi wetu kuhudhuria.
Kuna umuhimu kwa sheria kutumika kutamka shughuli rasmi ambazo viongozi wa ngazi ya Taifa wanapaswa kuhudhuria ili kupunguza mlolongo wa shughuli ambazo tunaoona zinazinduliwa na viongozi hawa. Hili likifanyika, litapunguza gharama kwa serikali na pia kuwapa muda mkubwa zaidi viongozi wetu kubaki kwenye sehemu zao za kazi na kusimamia vyema shughuli za serikali.
Kama nilivyosema awali, hapa nimetoa mifano ya viongozi wa kitaifa kwa sababu ndiyo mifano iliyo rahisi kuitoa. Lakini hili ni tatizo lililopo katika ngazi zote, kuanzia mawaziri mpaka watendaji wa vijiji.
Watanzania nao wabadilishe fikra kuwa haiwezekani kuchapa kazi bila kufanya uzinduzi.
Sunday, March 17, 2013
Tathmini ya muziki wa Tanzania mwaka 2012 (sehemu ya pili kati ya nne)
Katika makala hii nitakayoitoa katika sehemu nne, mwanamuziki mashuhuri John Kitime, anafanya tathmini ya hali ya muziki Tanzania mwaka 2012.
******************************************
Tathmini ya muziki wa Tanzania mwaka 2012
makala ya John Kitime
(Sehemu ya pili kati ya sehemu nne)
Muziki
asili pia umekosekana kwenye vyombo vya habari kwa kuwa si vikundi vingi vya
muziki huu vyenye uwezo wa kulipia gharama za studio ambao muziki huu
unastahili kurekodiwa. Studio nyingi zimejengwa kwa ajili ya muziki wa aina ya
Bongoflava tu. Zile studio za kuweza kuruhusu kundi la muziki wa asili kurekodi
gharama yake huwa ni kubwa sana.
Kundi
la Makirikiri lilitakiwa kuwa elimu tosha kwa wasanii wa muziki wa kiasili,
kuwa na muziki huo ukifuata taratibu nzuri ya kurekodiwa unauza vizuri sana. Bahati
mbaya kuna vikundi sasa vimeacha muziki na ngoma zao, vinaiga uchezaji wa Makirikiri.
Pengine
watu watasema nimesahau muziki wa kwaya; sijausahau. Kwa kweli muziki huu
umebaki hasa kwenye muziki wa injili.
Hapo zamani ulikuwa ukitumika sana kwenye siasa na kampeni , lakini kwa mwaka
2012 hali imekuwa mbaya kwa muziki huu.
Pamoja
na kuwa wengine wangeweza kusema tunasonga mbele katika muziki, kwangu mimi
naona tunarudi nyuma kitaaluma. Tasnia inaingiza pesa nyingi zaidi, na hata
kuna wasanii walioingiza pesa nyingi sana, lakini kwangu hilo si kipimo cha maendeleo katika
tasnia hii.
Kama
nilivyoanza kusema washika maikrofon wamekuwa ndiyo alama ya muziki wa Tanzania.
Muziki ni zaidi ya kuimba. Katika kuimba sauti nzuri ya muimbaji ni muhimu, na
ninashukuru kwa hilo tunao waimbaji wazuri wengi sana, lakini ule muziki
unaomsindikiza muimbaji ni muhimu sana kwani ule hauna mipaka wala lugha, na
ndio unaoweza kutufungulia mlango wa soko la kimataifa. Wengi tunapenda sana
muziki wa kutoka Kongo, Nigeria, Afrika Kusini; pamoja na kuwa hatujui hata moja
wanaloliongelea tunaupenda muziki huo kutokana na mpangilio wa vyombo vyao.
Kutokujali
wapigaji katika mfumo wa nchi yetu ndiyo unatupelekea kuwa watu wa ‘copy and paste’ wa upigaji wa muziki wa
nchi nyingine. Ukiorodhesha nyimbo zote zilizotikisa nchi hii kwa mwaka 2012
utagundua asilimia kubwa ya muziki uliotumika ulikuwa ni wa kunakili kutoka
muziki wa nchi nyingine, Nigeria, Congo na Afrika Kusini ndiyo wamekuwa waalimu
wetu wakuu.
Ushauri
kwa ma-producer wa Bongoflava: kuangalia pia muziki wetu wa asili humu ndani ya
nchi ili tuje tumalize 2013 na kitu chetu ambacho Wanaigeria, Wakongo nao pia
waige toka kwetu. Inawezekana sana maana wimbo wa Weekend wa Afro70 uliwahi
kuweko katika kumi bora 1972, Nigeria.
Muziki
wa injili pamoja na kuwa ndiyo unaotegemewa kutufundisha maadili, ulikuwa na
kasoro moja kubwa nayo ni kukosa maadili kwa ku-copy na ku-paste. Nyimbo
nyingi zilizokuwa maarufu na kuteka hisia za maelfu ya watu zilikuwa ni kuiga
moja kwa moja kutoka Afrika ya kusini. Najiuliza je ndiyo kilichopunguza moto wa
muziki huu 2012? Kulikuwa hakuna za kukopi? Wanamuziki wa injili kama ilivyo
kwa ushauri kuhusu Bongoflava, ni muda wa kurudi nyuma na kutumia rasilimali ya
utamaduni iliyoko kuleta mabadiliko na kukuza soko la muziki huo.
(itaendelea)
Taarifa zinazohusiana na hii:
Subscribe to:
Posts (Atom)
