Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, January 8, 2013

Lugha yetu Kiswahili

Miaka mingi iliyopita wakati nafanya kazi Dar es Salaam nilikuwa natoa huduma ya kufasiri lugha ya Kitaliani kutoka kwenye nyaraka mbalimbali zenye maandishi ya Kiingereza na Kiswahili. Nilipata kusoma nchini Italia miaka mingi iliyopita ambako nilijifunza lugha ya huko.

Kwa kuwa mimi siyo mtaalamu wa lugha mara kadhaa nilitembelea ofisi ya Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) ambayo ilikuwa jirani na ofisi yangu ili kupata ufafanuzi wa maneno ambayo sikuwa na hakika niliyatumia kwa usahihi kwenye ile kazi ya tafsiri.

Wakati mmoja mtaalamu mmoja wa lugha huko BAKITA alinifahamisha kuwa maana sahihi kwa Kiingereza ya neno "tafsiri" ni translation na kuwa "kufasiri" ilikuwa na maana to translate. Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa maelezo yake, haikuwa sahihi kutamka: "Leo nimetafsiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza. Ilikuwa sahihi kusema: "Leo nimefasiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza. Hii ndiyo hoja yangu niliyokusudia kuiwasilisha leo hapa ambayo nimelazimika kuibadili baada ya kufungua kamusi ili kuhakikisha kuwa ninayotaka kuandika ni sahihi.
Nilichogundua ni tofauti kidogo na yale niliyoambiwa kule BAKITA. Ni kweli kuwa neno lina maana ile niliyofafanuliwa na yule mtaalamu. Lakini nimegundua sasa, kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili - Kiingereza toleo la 2001 iliyochapishwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ni sahihi pia kusema: "Leo nimetafsiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza."

Hisia zangi ni kuwa matumizi yasiyo sahihi yaliendelea kwa muda mrefu na kwa watumiaji wengi sana wa lugha ya Kiswahili na kuwafanya waandaaji wa Kamusi kuhalalisha matumizi mapya ya neno hilo.

Taarifa zinazohusiana na taarifa hii:
http://muhunda.blogspot.com/2010/10/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2012/11/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2010/04/lugha-yetu-kiswahili.html

No comments: