Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, March 9, 2012

"Asilimia 98 ya Watanzania hawaheshimu sheria"

Kuna wakati mmoja, nadhani imepita miaka mitatu sasa, nilisikia mahojiano kwenye kipindi cha redio ambapo kamanda mmoja wa polisi wa mkoa alisema kuwa asilimia 98 ya Watanzania hawaheshimu sheria. Sikumbuki alikuwa ni nani na alikuwa wa mkoa upi.

Siamini kama alifanya utafiti wowote kabla ya kutamka hivyo, lakini kwa kuwa ni kamanda wa polisi tunaweza kuamini kuwa uzoefu wake unampa nafasi ya kutamka jambo ambalo linaweza kuwa sahihi kwa kiasi kikubwa.

Kwa hesabu za wakati ule ilikuwa ni kasi cha Watanzania laki saba tu ndiyo walibaki kuheshimu sheria za nchi yetu.

Ingefaa pia kuamini kuwa viongozi wetu, wale ambao wanapaswa kuongoza wananchi kuheshimu na kutii sheria, nao pia ni miongoni mwa hao laki saba. Kama si hivyo, hatufiki huko tuendako.

No comments: