Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, March 11, 2012

Tatizo la matandao Butiama linaelekea ukingoni

Watumiaji wa mtandao wa Internet Butiama si wengi lakini wachache tuliopo hupata shida kubwa sana kupata mawasiliano ya uhakika.
Kasi ya mtandao kwa kutumia huduma za mtandao za kampuni za simu za kiganjani ni ghali na aghalabu kasi ni ndogo sana. Kampuni nyingine hazitaki hata kuleta hiyo huduma. Nimekuwa nawabembeleza Zantel kwa zaidi ya miaka mitatu kuanzisha hiyo huduma Butiama lakini hawajaamua kuianzisha mpaka sasa.

Sasa nimepata taarifa kuwa mbunge wa Musoma Vijijini, Mhe. Nimrod Mkono, amewasilisha maombi serikalini ili mkongo wa Taifa wa mtandao uletwe pia Butiama. Katika maelezo yake Mhe. Mkono ameeleza kuwa Butiama sasa ni wilaya rasmi ya Serikali ambapo kuna shule kadhaa na kwa sababu hiyo anaona umuhimu wa kupata huduma hii muhimu.

Sent from Samsung Mobile

No comments: