Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, March 6, 2012

Selemani Galile kupambana na Thomas Mashali kuwania ubingwa wa TPBO Aprili 9

Mkanda wa ubingwa wa ngumi za kulipwa wa TPBO (Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania) katika uzito wa "middleweight" unatarajia kuwaniwa April 9 mwaka huu Dar es Salaam. Bado haijafahamika sehemu ambapo pambano hilo litafanyika.
Mkanda huo ambao upo wazi utawaniwa na bondia Thomas Mashali na Selemani Galile.

Galile amesema amejiandaa vyema kwa ajili ya kunyakua mkanda huo:
"Naendelea kufanya mazoezi yangu kwa ajili ya kuwania mkanda huu ambao ninaamini utaweza kunitambulisha ubora wangu katika tasnia hii ya masumbwi,"alisema Galile.

Alisema mpinzani wake Mashali hana hofu naye kwa kuwa mchezo huo huamua nani mkali atakayetwaa ubingwa wakati wakiwa ulingoni na si nje ya hapo na kwa sasa anasema amepata staili mpya za mabondia wa dunia.

Picha na taarifa kwa hisani ya superboxingcoach.

No comments: