Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, January 3, 2013

Taarifa ya Serikali kufafanua kuhusu miradi ya utafutaji na uvunaji wa gesi asilia nchini


****************************************************
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA NISHATI NA MADINI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUFAFANUA KUHUSU MIRADI YA
UTAFUTAJI NA UVUNAJI WA GESI ASILIA NCHINI

1.0   UTANGULIZI

Wizara ya Nishati na Madini inapenda kutoa ufafanuzi wa miradi ya Gesi Asilia ambayo itatekelezwa kwa kushirikiana na wawekezaji katika Sekta ndogo ya Gesi Asilia na kueleza manufaa makubwa  yatakayopatikana kwa wananchi wote wa Tanzania wakiwemo wale wa Mikoa ya Mtwara na Lindi.

Siku ya Alhamisi, tarehe 27 Disemba 2012, baadhi ya Vyama vya Siasa vya Upinzani viliratibu na kuhamasisha baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara, wengi wao wakitokea Mtwara Mjini kufanya  maandamano ya kudai raslimali ya Gesi Asilia iwanufaishe wakazi wa Mtwara na kupinga mradi mkubwa wa ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam. Wizara ya  Nishati  na Madini inapenda kutoa taarifa ifuatayo kwa Wa-Tanzania wote kwa kupitia vyombo vya habari.

Tokea Uhuru, uchumi wa Tanzania umetegemea kilimo cha mazao ya biashara kama vile katani (Tanga na Morogoro), pamba (Mwanza, Mara na Shinyanga), kahawa (Kilimanjaro, Kagera, Ruvuma  na Mara),  chai (Iringa) na tumbaku (Tabora). Fedha za mazao haya zimewanufaisha wakazi wa mikoa yote ya nchi yetu   bila ubaguzi wo wote wala wakulima wa kutoka       mikoa    hiyo     hawajawahi     kufanya        maandamano  wakidai
upendeleo (dhidi ya Wa-Tanzania wengine) wa aina yo yote ile.

1

Mapato   yatokanayo na uchimbaji wa dhahabu (Mwanza, Geita, Mara, Shinyanga  na  Tabora),  almasi  (Shinyanga)  na  tanzanite   (Manyara) yamewanufaisha Wa-Tanzania wote bila ubaguzi wo wote ule! Minofu ya samaki wa Ziwa Victoria (Mara, Mwanza na  Kagera) imeliingizia Taifa letu fedha nyingi ambazo zimetumiwa na wakazi wa nchi nzima bila ubaguzi wo wote.

Aidha kuna mikoa ambayo inazalisha mazao ya chakula kwa wingi kwa manufaa ya Wa-Tanzania wote. Mahindi kutoka Rukwa, Mbeya, Ruvuma na Iringa yanasafirishwa kwenda mikoa yote ya nchi yetu bila kujali eneo yanakolimwa na wakazi wa mikoa hiyo hawajawahi kudai mahindi hayo ni kwa ajili ya watu wa mikoa hiyo pekee. Sukari ya Kilombero, Mtibwa na Kagera inatumiwa na wakazi  wa mikoa yetu yote bila ya kuwepo madai ya mikoa inayozalisha sukari hii kupewa upendeleo wa  aina yo yote ile. Maji ya Mto Ruvu yanatumiwa na wakazi wa Dar Es Salaam bila manunguniko yo  yote kutoka kwa wakazi wa eneo la chanzo cha Mto Ruvu.

Umeme wa kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi (Dodoma na Morogoro), Hale (Tanga), na Nyumba ya Mungu (Kilimanjaro) unatumiwa na wakazi wote wa Tanzania bila ubaguzi au malalamiko ya  wenyeji  wa sehemu ambazo umeme huo unafuliwa na kusafirishwa kwenye Gridi ya Taifa. Kwa hiyo, kutokana na mifano hii michache, ni wajibu wa wazalendo na wapenda maendeleo wa kweli na hasa Wa-Tanzania wanaopinga ubaguzi wa aina yo yote ile kujiuliza kwa kina sababu zilizopelekea Vyama Siasa vya      Upinzani         kupanga,  kuhamasisha,                     kushabikia   na    kuongoza maandamano ya tarehe 27 Disemba 2012 pale Mtwara Mjini.

2.0   RASLIMALI YA GESI ASILIA TANZANIA

Gesi Asilia ilianza kugundulika hapa nchini tangu mwaka 1974 kwenye Kisiwa  cha  Songo  Songo,  Mkoani  Lindi.  Baada  ya  hapo  Gesi  Asilia imegundulika maeneo ya Mtwara Vijijini, yaani Mnazi  Bay (1982) na Ntorya (2012), Mkuranga (Pwani, 2007), Kiliwani (Lindi, 2008). Kiasi cha
Gesi Asilia iliyogunduliwa katika maeneo haya inakadiriwa kuwa Futi za

2

Ujazo  Trilioni   4.5   –  8.  Katika  kipindi  cha  miaka  mitatu  iliyopita, kumekuwa na kasi kubwa ya utafutaji Mafuta na Gesi Asilia uliojikita zaidi  kwenye  maji  ya  kina  kirefu  cha  bahari.  Kiasi  cha  Gesi  Asilia iliyogundulika katika kina kirefu cha maji inafikia  takribani Futi za Ujazo Trilioni 27. Kiasi cha wingi wa Gesi Asilia yote iliyogunduliwa nchi kavu na baharini inafikia takribani Futi za Ujazo Trilioni 35.

Kufuatana  na  Sheria  za  nchi  yetu  zinazotumiwa  kugawa mipaka  ya mikoa iliyopo kando  kando mwa bahari (isivuke 12 nautical miles au
22.22 km kuingia baharini), Gesi Asilia iliyogunduliwa hadi sasa katika
Mkoa wa Mtwara pekee ni asilimia 14 tu ya gesi yote iliyogundulika nchini. Kwa kutumia kigezo hicho cha Sheria za mipaka ya ki-utawala ya mikoa yetu, Lindi inayo 7% ya gesi yote, Pwani 1% na huku Kina Kirefu cha Bahari (Deep Sea) ndicho chenye gesi nyingi (78%) kuliko mikoa yote    ikiwekwa pamoja!         Kwa          hiyo,       hakukuwa  na               haja         ya   kufanya maandamano kwa sababu Gesi Asilia nyingi inapatikana kwenye bahari ya kina kirefu ambayo iko  ndani ya mipaka ya nchi yetu bila kujali mipaka ya mikoa yetu. Isitoshe Gesi Asilia imegundiliwa kwenye miamba tabaka (sedimentary rocks) yenye umri wa Miaka kati ya Milioni 199.6 hadi 23.03. Mipaka ya Bara la Afrika, ya nchi yetu na ile ya mikoa yetu haikuwepo wakati huo!

Utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia pia unaendelea tukiwa wa mategemeo makubwa  ya  upatikanaji  wa  raslimali  hizi  katika  Mikoa  ya  Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Manyara, Kigoma, Mbeya, Njombe,  Rukwa, Katavi, Morogoro na Tabora pamoja na kwenye kina kirefu cha maji baharini kuanzia  mpaka  wetu  na  Msumbiji  hadmpaka     wetu  na   Kenya. Hatutarajii  mikoa  hii  nayo  ifanye  maandamano  ya  kutaka  kuhodhi raslimali za Gesi Asilia na Mafuta zitakapogunduliwa mikoani mwao.

3.0   MATUMIZI   YA   GESI   ASILIA   YA   MNAZI   BAY   (MTWARA)   NA SONGO SONGO (LINDI)

Mpaka hivi sasa Gesi Asilia inayozalishwa na kutumika nchini ni kutoka
Mnazi Bay (Mtwara Vijijini) na Songo Songo (Kilwa, Lindi). Gesi ya Mnazi

3

Bay kwa sasa huzalisha umeme kwa ajili ya Mikoa ya Mtwara na Lindi tu. Mitambo ya kufua  umeme kutokana na Gesi Asilia iliyopo Mtwara Mjini inao uwezo wa kuzalisha MW 18 lakini  matumizi ya umeme ya Mikoa ya Mtwara na Lindi haijavuka MW 12. Umeme huo wa Mtwara unafuliwa na TANESCO huku Kampuni za Wentworth na Maurel & Prom zikizalisha Gesi Asilia            (inayotumiwa na TANESCO) kiasi cha Futi za Ujazo Milioni 2 kwa siku. Ikumbukwe kwamba  ufuaji wa umeme wa hapo    Mtwara          Mjini      ulikuwa mikononi         mwa   Kampuni ya  Artumas iliyofilisika.  Tangu   Desemba   2006   hadi   leo   hii   kiasi   cha   gesi kilichotumika kufua umeme kwa ajili ya mikoa hiyo miwili ni chini ya asilimia 1 ya gesi yote iliyogundulika  Mnazi Bay (Mtwara Vijijini). Vilevile  ikumbukwe kwamba  kuna  visima  vinne  vya  Gesi  Asilia  pale Mnazi Bay (Mtwara Vijijini) na kinachotumika kwa sasa na tena kwa kiwango cha chini kabisa ni kimoja tu!

Aidha ni vizuri ndugu zangu Wa-Tanzania wakaelewa kuwa Gesi Asilia hii  inatafutwa  na  kuchimbwa na  wawekezaji  wenye  mitaji  mikubwa, wataalamu na teknolojia ya utafutaji na uchimbaji wa Gesi Asilia ambao wanapaswa kurejesha mitaji yao. Uchorangaji wa kisima kimoja  cha utafutaji wa Gesi Asilia nchi kavu unahitaji Dola za Marekani Milioni
40, na kwenye kina kirefu cha maji baharini zinahitajika zaidi ya Dola za       Marekani    Milioni    100.    Ikumbukwe       kwamba, Serikali    kwa kushirikiana na Shirika la Mafuta la Tanzania (TPDC), inatumia fedha za walipa  kodwa   nchi nzima  kwa  shughuli     za   kuvutia,            kuratibu       na kusimamia utafutaji na uendelezaji wa Gesi Asilia nchini kote ikiwemo Mikoa            ya  Mtwara    na             Lindi.         Walipa   kodi            Wa-Tanzania        bado hawajalalamika wala hawajafanya maandamano ya kudai            fedha zao za kodi zisitumike huko Mtwara!

Ni muhimu pia tukaelewa kwamba Gesi Asilia iliyopo Mnazi Bay (Mtwara Vijijini) inazalisha umeme  peke yake kwa ajili ya Mikoa ya Mtwara na Lindi.  Gesi  Asilia  ya  Songo  Songo  (Kilwa,  Lindi)  ndiyo  inayotumika kuzalisha                 umemkwa  ajili  ya  Gridi  ya  Taifa,  na  pia  kwa  ajili  ya
wananchi  wa  Kisiwa  cha  Songo  Songo  (Lindi),  maeneo  ya  Somanga

4

Fungu  (Lindi)  na  viwandani  (Dar  Es  Salaam)TangOktob2004 ambapo mitambo ya kufua umeme ilipoanza kazi hadi leo hii, kiasi cha Gesi Asilia ya Songo Songo kilichotumika ni asilimia 7 tu ya Gesi Asilia yote iliyogunduliwa huko. Kwa hiyo, takwimu zinaonyesha kwamba hata uchumi wa Jiji la Dar Es Salaam unatumia kiasi kidogo sana cha Gesi Asilia  (7%)  iliyopo  Songo  Songo  (Kilwa,  Lindi).  Ikumbukwe  kwamba waajiriwa kwenye viwanda vya Dar Es Salaam wamo wanyeji wa kutoka Mtwara       Mjini    ambako     maandamano     yalifanyika     na       vilevile   wamo wafanyakazi ambao ni wanachama wa Vyama vya Siasa  vya Upinzani vilivyopanga, ratibu na kushabikia maandamano ya Mtwara Mjini ya tarehe 27 Disemba 2012.

4.0   MIPANGO YA MATUMIZI YA GESI ASILIA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA 5 HADI 10

(a)  Ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia hadi Dar Es Salaam:

Kuuza Gesi Asilia Jijini Dar es Salaam, kitovu cha uchumi wa Tanzania (80% ya  mapato ya nchi yetu yanazalishwa Dar Es Salaam) ni uamuzi mzuri wa ki-uchumi. Tayari kuna viwanda
34 vinatumia Gesi Asilia  ambavyo vinahitaji kupanua shughuli zao endapo gesi zaidi  itapatikana. Soko kubwa la Gesi Asilia lipo        tayari  Dar   es  Salaam  (na  siyo   Mtwara),  ambapo  ipo mitambo  ya   kufuumeme   kwa   kutumia         mafuta. Serikali inatumia fedha nyingi za kigeni kununulia mafuta ya kufua umeme tunaoutumia kila siku. Takribani   Dola za Marekani Bilioni  Moja  (sawna   ShilingTrilioni    1.6)   kwa  mwaka zitaokolewa kutokana na mitambo iliyopo nchini ikifua umeme kwa kutumia Gesi Asilia na kuachana na mafuta ambayo ni ya bei  kubwa  sana.  Bei  ya  umeme  kwa  uniti  moja  (KWh)  ya umeme unaofuliwa kutumia dizeli na mafuta ya aina nyingine ni kati ya Senti za Marekani 30 hadi 45 na huku bei ya      uniti moja hiyo hiyo ni Senti za Marekani 6-8 kwa umeme utokanao na Gesi Asilia na zinapungua na wakati wa matumizi.

Vilevile, takribani Dola za Marekani millioni 202 kwa mwaka zitaokolewa iwapo Jiji  la  Dar Es Salaam litatumia Gesi Asilia badala ya mafuta katika magari, taasisi na majumbani. Fedha

5

hizi zikiokolewa zitatoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa Taifa letu kwa manufaa  ya Wa-Tanzania wote wakiwemo wale waliondamana na wale walioratibu maandamo ya Mtwara Mjini ya tarehe 27 Disemba 2012.

(b) Umeme mwingi zaidi kutokana na Gesi Asilia:

Bomba la Gesi Asilia linalojengwa litasafirisha gesi nyingi zaidi ambayo itawezesha mitambo mipya itakayojengwa Kinyerezi (Dar Es Salaam) kufua umeme wa zaidi ya MW 990. Umeme mwingine utafulia  Somanga  Fungu  (Lindi)  wa  kiasi  kisichopungua  MW
520.

(c) Usafirishaji na usambazaji wa umeme nchini mwetu:

Dar   es   Salaam   ndiko      kuna   miundombinu  mikubwa   ya usafirishaji  na  usambazaji  wa  umeme  kuliko  mikoa  mingine yote, hivyo ni uamuzi wa ki-uchumi unaotulazimisha kusafirisha Gesi Asilia kutoka Mikoa ya Lindi na Mtwara na kuipeleka Dar Es Salaam ambako itatumika kufua umeme, na kutumika moja kwa moja viwandani, majumbani na kwenye magari.

(d) Kwa  kuzingatia  mahitaji  ya  Gesi  Asilia  yatakayojitokeza: Bomba  la kusafirisha  gesi litawekewa matoleo ya kuchukulia gesi (tie-off) katika maeneo ya Mtwara, Lindi, Kilwa na Mkuranga ili kuhakikisha kuwa miji hii inakuwa na Gesi Asilia ya uhakika wakati wowote itakapohitajika. Kwa hiyo kuweka mitandao ya usambazaji        wa gesi   kutoka              kwenyBomba           la           Gesi       Asilia linalojengwa kutarahisisha matumizi ya Gesi Asilia viwandani na majumbani katika Mikoa ya Mtwara na Lindi, na kwenye mikoa mingine kwa siku za baadae.

(e)Serikali   imetenga   maeneo katika pwani ya Mikoa ya Kusini (Lindi na           Mtwara)         kwa  ajili  ya   uanzishwaji      wa           maeneo             ya viwanda    (Industrial Parks/Estates)   vikiwemo      viwanda vya mbolea,  Liquefied    Natural    Gas   (LNG)   na   Petrochemicals. Ujenzi wa kiwanja cha sementi uko katika hatua za mwisho za maandalizi.
(f) Ili kutengeneza mazingira mazuri ya biashara ya Gesi Asilia na Mafuta kwa kampuni za  huduma, malighafi na vitendea kazi, Serikali imetenga eneo maalumu Mtwara,  ambalo  litawekewa

6

miundombinya   msingi   ili   kutoa   vivutio  mbalimbali  kwa makampuni hayo. Eneo hilo litapewa hadhi ya Ukanda Huru wa Bandari (Freeport Zone).

Ni lazima shughuli za kusafisha na kusafirisha Gesi Asilia zitatoa ajira katika  maeneo  husika.  Kwa  mfano  kwa  mitambo  ya  kusafishia  gesi inayojengwa Madimba (Mtwara Vijijini) na SongoSongo (Kilwa, Lindi), kila mtambo utahitaji wafanyakazi na wengine watatoka Mikoa ya Lindi na Mtwara.

Watanzania  wanakumbushwa  kuwa  raslimali  zilizopo  nchini  ikiwemo gesi asilia, madini, makaa  ya mawe, wanyama pori, misitu, milima ya utalii, mito, maziwa, bahari n.k ni za Wa-Tanzania wote kwa mujibu wa Katiba ya             Jamhuri          ya    Muungano   wa   Tanzania.   Raslimali   hizi zinapatikana,  zinatunzwa  nkuzalishwmaeneo  mbalimbali  nchini mwetu na mapato yake yanatumika kwa maendeleo ya Wa-Tanzania wote bila kujali maeneo raslimali hizo zilipo.


Tusikubali kuvunja nchi yetu vipande vipade kwa kisingizio cha raslimali zilizopo mikoani  mwetu. Tusikubali kuvunjavunja mikoa yetu    kwa          kisingizio             cha   raslimali   zilipo    kwenye    wilaya   zetu. Tusikubali kuvunjavunja  wilaya zetu kwa kisingizio cha raslimali zilizopo kwenye tarafa zetu. Tusikubali  kuvunjavunja tarafa zetu kwa kisingizio cha raslimali zilizopo kwenye kata zetu. Tusikubali kuvunjavunja kata zetu kwa kisingizio cha raslimali zilizopo kwenye vijiji vyetu na mitaa yetu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, DUMISHA UHURU NA UMOJA WETU 
Prof Dr Sospeter Muhongo (Mb)
WAZIRI YA NISHATI NA MADINI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA










7

No comments: