Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, September 12, 2010

Jagwa Music waendeleza rirandi nchini Denmark

Jagwa Music ni kikundi ambacho kinapiga muziki wa Mchiriku, au Mnanda, kama vijana wengi wanavyopenda kuuita. Wasanii hawa sasa hivi wako katika ziara ya maonyesho mawili nchini Denmark.

Jana usiku walianza makamuzi ya kasi kubwa. Leo hii, kuanzia saa mbili usiku watakuwa katika mji wa Roskilde kwa ajli ya makamuzi mengine.

Ziara hii, itayakayohitimishwa tarehe 13 Septemba, ni kwa ajli ya kujitangaza kwa ajili ya maandalizi ya ziara nyingine ndefu hapo mapema mwaka 2011.


Waratibu wa safari hii ni kampuni ya Jahazi Music, na kwa maandalizi yote nchini Tanzania wanashirikiana na kampuni ya Maisha Music.


Mwenyeji wa ziara hii nchini Denmark ni kampuni ya GlobalCPH. Kikundi hiki kinamilikiwa na George Sultani Jolijo, na kusimamiwa na kampuni ya Maisha Music Tanzania Limited.

No comments: