Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, September 15, 2010

Mlima Kilimanjaro Novemba

Mwezi Novemba, mwaka huu, natarajia kupanda Mlima Kilimanjaro kwa mara ya tatu chini ya mpango wa kuchangisha pesa za hisani katika tukio ambalo linaitwa The Mwalimu Nyerere Charity Climb 2010.

Mwaka 2008 nilifanikiwa kuchangisha zaidi ya Sh.20/- milioni ambazo zilichangia ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Chief Edward Wanzagi iliyopo Buturu, Mkoa wa Mara.

Wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana ya Chief Edward Wanzagi, mbele ya shule yao.

Mwaka 2009 nilipanda tena Kilimanjaro nikikusudia kuchangisha pesa kwa ajili ya asasi ya mjini Musoma, Community Alive, inayojishughulisha na kutoa msaada kwa watoto yatima ambao wazazi wao wamekufa kwa UKIMWI. Pamoja na kupata msaada mkubwa wa vyombo vya habari katika kuhamasisha uchangiaji, pesa zilizoahidiwa zilivuka kwa kiasii kidogo tu Sh.2/- milioni. Na sehemu yote ya hizo ahadi haikulipwa.

Mwaka huu bado haijaamuliwa mchango utakuwa kwa ajili ya madhumuni gani.

Mwaka 2008 nilipanda Kilimanjaro na raia wa Vietnam, Le Huyn. Mwaka jana nilipanda na Watanzania wawili: Notburga Maskini wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa), pamoja na Gerald Hando wa Clouds FM.

Mwaka huu Gerald Hando amesema atashiriki tena. Kundi zima litashirikisha wafuatao:

1. Jaffar Amin 
Jaffar Amin, akijaribisha miwani ya kuvaa wakati wa kupanda Mlima Kilimanjaro
2. Muhidini Issa Michuzi wa Blogu ya Jamii & 3. Fred Fredwaa wa Radio Free Africa
Muhidini Michuzi, na Fred Fredwaa Fidelis

4. Philipp Kissanga, raia wa Austria

Phillipp Kissanga, kulia
5. Matare Nyerere
Matare (wa tano kutoka kushoto) akiwa na timu yake ya mpira ambayo kiwanja cha nyumbani ni kwenye klabu ya Tazara, Dar es Salaam 
6. Amrani Batenga (Mfanyabiashara wa Mwanza)
7. Cutlat Mazengo (National Insurance Corporation)
8. Gerald Hando (Clouds FM)
9. Prof. Khoti Kamanga (Chuo Kikuu cha Dar es Salaam)
10. Mustafa Othim (kutoka Nakuru, Kenya)
11. Salum Mwaimu (wa Channel10)
12. Mary Kalikawe (Mkurugenzi wa Kiroyera Tours)
13. Stefan Joham (raia wa Austria)
14. Makongoro Nyerere (Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mara)
15. William Rutta (Meneja, Kiroyera Tours) 

William Rutta
Katika taarifa zijazo, nitatoa maelezo na picha ya safari yangu ya mwaka 2008 kupanda Mlima Kilimanjaro.

Makala inayohusiana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2010/09/kisa-cha-kuacha-kuvuta-sigara-ari-yangu.html

No comments: