Jaji Augustino Ramadhani akipata maelezo toka kwa muongozaji wageni wa Makumbusho ya Mwalimu J.K. Nyerere ya Butiama wakati wa ziara yake ya Butiama. |
Tuesday, January 29, 2013
Wageni wa Butiama: Jaji Augustino Ramadhani
Kati ya wageni ambao wametembelea Butiama ni pamoja na aliyekuwa Jaji Mkuu Augustino Ramadhani. Alitembelea Butiama wakati akiwa Jaji Mkuu.
Mapema mwaka 2012 Jaji Ramadhani aliteuliwa kuongoza jopo la majaji waliochunguza tukio la Naibu Jaji Mkuu wa Kenya, Nancy Baraza, aliyetuhumiwa kumtishia kwa silaha mlinzi mmoja wa duka moja la jijini Nairobi.
Amani Millanga ahoji ukodishwaji wa maeneo makubwa ya ardhi kwa wawekezaji (sehemu ya pili kati ya sehemu tatu)
Katika sehemu ya pili ya makala yake hii ambayo nitaitoa katika sehemu tatu, Amani Millanga anahoji ukodishaji wa maeneo makubwa ya ardhi kwa wawekezaji na, kwa maoni yake, utaratibu huu unaturejesha kwenye ukoloni.
**********************************************************
Mali ya Taifa (sehemu ya pili)
Na Amani Millanga
Hoja ya pili kwamba “ardhi
bado ipo” ni hoja ambayo inatolewa bila kuangalia kwa mapana na kina athari za
ukodishaji ardhi kwa wageni. Mwaka 1961 idadi ya watu ilikuwa ni milioni
kumi. Miaka 50 baadaye Tanzania ilikuwa na watu milioni 45. Hii ina maana
kwamba idadi ya watu imeongezeka mara 4.5 toka milioni kumi hadi milioni 45
mwaka 2011.
Kwa msingi wa hesabu hii
ina maana kwamba katika miaka 50 ijayo (mwaka 2061) Tanzania itakuwa na
watu milioni 45 x 4.5 = watu milioni 202.5. Je watu hawa wataishi wapi?
Watajimudu vipi? Watapata wapi ardhi ilhali sehemu kubwa ya ardhi yetu itakuwa
imekodishwa kwa wageni kwa miaka 99?
Hapo ina maana kwamba
utakuwa na miaka 49 ya wawekezaji kumaliza muda wao. Katika hii miaka 49 (yaani
mwaka 2110) idadi ya Watanzania itakuwa imeongezeka tena mara 4.5 (tukitumia
msingi wa hesabu yetu wa ongezeko la watu wa mara 4.5) kwa maana kwamba watu
milioni 202.5 x 4.5 = Tanzania itakuwa watu milioni 911.25 Hadi idadi ya watu
inafikia kiwango hiki cha milioni 202.5 katika miaka 50 ijayo (mwaka 2061) au
milioni 911.25 katika miaka 99 ijayo (mwaka 2110) tufahamu kwamba itakuwepo
vita kali sana ya wananchi kuidai ardhi yao. Wengi watakufa bure kwa sababu ya
maamuzi yasiyo ya kizalendo yanayotolewa hivi sasa ya kukodisha ardhi.
Mtu anaweza kusema ni
jambo ambalo haliingii akilini kwamba Tanzania katika miaka 99 ijayo itakuwa na
watu milioni 911.25. Lakini hili ni jambo ambalo linawezekana tukidurusu
historia ya ongezeko la watu duniani. Ukiziangalia takwimu za
ongezeko la idadi ya watu duniani katika miaka 2000 iliyopita utaona kwamba
ongezeko kubwa la watu limekuwepo katika miaka 200 tu iliyopita. Mwaka 1800
dunia ilikadiriwa kuwa na idadi ya watu bilioni moja na mwaka 1900 idadi ya
watu iliongezeka na kufikia bilioni moja na nusu. Tokea mwaka 1800 hadi mwaka
2000 idadi ya watu iliongezeka mara sita kufikia watu bilioni 6.1.
Katika kipindi cha miaka
12 tu yaani mwaka 2000 hadi mwaka 2012, idadi ya watu duniani imeongezeka kwa
kasi kubwa sana na imefikia watu zaidi ya bilioni 7.1 kwa mujibu wa tovuti http://www.worldometers.info/world-population/. Umoja wa Mataifa unakadiria idadi ya watu itakuwa
bilioni 9 ifikapo mwaka 2050 na ongezeko kubwa la watu liko Afrika, kusini mwa
Jangwa la Sahara, ambayo itakuwa na watu bilioni 2.756 mwaka 2050, likiwa ni
ongezeko la watu bilioni 1.9 kutoka watu milioni 856 mwaka 2010 (ongezeko la
watu zaidi ya mara mbili katika miaka 40) na 39% ya watu wenye umri kati ya miaka
15 hadi 24 duniani watakuwa Waafrika ifikapo mwaka 2100 kutoka 14% mwaka 2010.
Kwa hiyo upo ushahidi wa
kutosha kwamba katika miaka 50 ijayo Tanzania itakuwa na watu milioni 202.5.
Ardhi haiongezeki. Sasa katika hizo hekta milioni 44 tulizonazo ambazo kwa
idadi ya watu ya milioni 45 ya mwaka 2011 ni sawa na hekta 0.977 kwa kila Mtanzania
(kwa maana ya hekta milioni 44 gawa kwa watu milioni 45). Je hamuoni kwamba
wastani huo wa ardhi kwa kila mtanzania utakuwa umeshuka sana katika miaka 50
ijayo?
Hesabu hii itatupa
mwanga: hekta milioni 44 gawa kwa watu milioni 202.5 utapata hekta 0.217 kwa
kila mtanzania. Je katika kasi hii ya kukodisha ardhi kwa wageni wastani huu wa
hekta 0.217 utakuwepo kwa kila mtanzania? Ardhi itapatikana wapi? Bila shaka
vijana watasimama kuidai ardhi tena kwa mabavu.
Ni ukweli usio na shaka
kwamba idadi ya watu wanaohama vijijini kwenda mijini inaongezeka lakini hii
haina maana kwamba katika miaka 50 ijayo 80% ya Watanzania itakuwa inaishi
mijini na 20% itakuwa inaishi vijijini. Katika miaka 50 iliyopita yamekuwepo
mabadiliko madogo sana ya watu kuhamia mijini ingawa kasi ya kuhamia mijini
inaongezeka lakini bado 80% na huenda hata zaidi wanaishi vijijini hivi sasa.
Kama hali itaendelea kuwa hivi, basi katika kujenga taswira ya hali ya mambo
itavyokuwa tunaweza kukadiria kwamba 50% ya Watanzania watakuwa wanaishi mijini
mwaka 2061. Hii ina maana kwamba watu milioni 202.5 gawa kwa mbili utapata
idadi ya watu 101.25 watakuwa bado wanaishi vijijini wakitegemea kilimo kama
ajira yao kuu.
Je tutakuwa na ardhi ya
kukidhi mahitaji ya watu hawa kwa mnasaba wa kasi ya ukodishaji ardhi iliyopo?
Hapa ndipo unahitajika umakini wa hali ya juu sana katika kuangalia hatima ya
Tanzania na watu wake. Kwa mtizamo uliopo sasa Tanzania ya 2061 itakuwa na
mgogoro mkubwa sana wa ardhi zaidi ya ule wa Zimbabwe.
Taarifa zinazohusiana na hizi:
http://muhunda.blogspot.com/2010/07/kaburi-la-mbaguzi-nambari-wani-cecil.html
Taarifa zinazohusiana na hizi:
http://muhunda.blogspot.com/2010/07/kaburi-la-mbaguzi-nambari-wani-cecil.html
Sunday, January 27, 2013
Kwenye soka huwa nashangilia wanyonge siku zote
Makala hii niliandika zaidi ya miaka mitatu iliyopita kwenye blogu yangu ya lugha ya Kiingereza. Nairudia hapa kwa wale ambao hawakupata fursa kuisoma wakati huo, tarehe 30 Juni 2009. Nimekosa kuangalia mapambano ya Kombe la Mataifa ya Afrika yanayoendelea sasa hivi nchini afrika Kusini lakini ningekuwa nafuatilia mashindano hayo ningekuwa nawapigia debe wanyonge, timu ambayo hakuna shabiki anatarajia itashinda.
*********************************************
Mimi siku zote hushangilia wanyonge, hususani kwenye michezo. Kwa hiyo nilifurahishwa Jumapili iliyopita nilipowasha televisheni na kushuhudia hali isiyo ya kawaida ambapo timu ya taifa ya Marekani ikiwa inaongoza kwa goli moja bila majibu na, kabla ya kipenga cha nusu ya kwanza kusikika, ikiongoza kwa magoli mawili dhidi ya miamba ya soka Brazil kwenye pambano la fainali za mabara la FIFA nchini Afrika ya Kusini.
Katika ulimwengu wa soka Brazil inatisha, ni taifa kubwa wakati Marekani ni bwana wadogo. Katika lugha ya vita na silaha Brazil ni mzinga wa upana wa milimita 130 wakati Marekani ni kama bastola ndogo isiyojaza hata mfuko wa shati. Kwa hiyo si ajabu kumsikia kocha wa Marekani Bob Bradely akisema baada ya timu yake kushindwa: "Ni matarajio yangu kuwa watu katika sehemu mbalimbali duniani wataona kuwa tunayo timu na wachezaji wazuri. Ni hatua kubwa kwetu."
Timu ya Taifa ya Brazil iliyoshinda Kombe la Dunia mwaka 1970 nchini Mexico. |
Timu nilizozishabikia kwenye mashindano zilikuwa mlolongo wa timu zilizoorodheshwa na FIFA kwa ubora lakini orodha ile ikiwa imewekwa kichwa chini miguu juu, yaani zile za mwisho ndiyo nilipendelea zaidi zishinde.
Katika kipindi cha pili Brazil walisawazisha mabao yote mawili na kuongeza bao la tatu la ushindi ambalo lilikuwa uthibitisho kuwa Brazil itabaki inatawala ulimwengu wa soka, angalau kwa sasa.
Habari njema kwa timu nyingine ambazo zitapambana na Brazil kwenye Kombe la Dunia la FIFA mwakani nchini Afrika ya Kusini ni kuwa bingwa wa FIFA wa mabara - ambapo mabingwa wa mabara wanapambana dhidi yao - hajawahi kutwaa ubingwa wa dunia mwaka unaofuata.
Katika kipindi cha pili Brazil walisawazisha mabao yote mawili na kuongeza bao la tatu la ushindi ambalo lilikuwa uthibitisho kuwa Brazil itabaki inatawala ulimwengu wa soka, angalau kwa sasa.
Habari njema kwa timu nyingine ambazo zitapambana na Brazil kwenye Kombe la Dunia la FIFA mwakani nchini Afrika ya Kusini ni kuwa bingwa wa FIFA wa mabara - ambapo mabingwa wa mabara wanapambana dhidi yao - hajawahi kutwaa ubingwa wa dunia mwaka unaofuata.
Taarifa zinazohusiana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2010/07/mada-yangu-ya-leo-ni-nani-ataibuka.htmlhttp://muhunda.blogspot.com/2010/06/hii-kali.html
Wednesday, January 9, 2013
Wageni wa Butiama: Mhe. Benjamin William Mkapa
Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa ametembelea Butiama mara nyingi, kabla na baada ya kustaafu kwake kama Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.
Kwenye picha hii ilikuwa mara yake ya mwisho kutembelea Butiama alipohudhuria mazishi ya Mzee Josephat Kiboko Nyerere, mdogo wake Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mzee Kiboko ni baba mzazi wa mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA).
Kwenye picha hii ilikuwa mara yake ya mwisho kutembelea Butiama alipohudhuria mazishi ya Mzee Josephat Kiboko Nyerere, mdogo wake Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mzee Kiboko ni baba mzazi wa mbunge wa Musoma Mjini, Vincent Nyerere (CHADEMA).
Amani Millanga ahoji ukodishwaji wa maeneo makubwa ya ardhi kwa wawekezaji (sehemu ya kwanza kati ya sehemu tatu)
Katika makala yake hii ambayo nitaitoa katika
sehemu tatu, Amani Millanga anahoji ukodishaji wa maeneo makubwa ya ardhi kwa
wawekezaji na, kwa maoni yake, utaratibu huu unaturejesha kwenye ukoloni.
Kwa mujibu wa takwimu za serikali, Tanzania
inazo hekta 44 milioni za ardhi nzuri ya kilimo. Kwa sasa ni asilimia 23 tu ya
ardhi hiyo inatumika kwa kilimo, ambayo ni sawa na hekta 10,120,000. Hii
ina maana kwamba tuna ziada ya hekta 33,880,000 (yaani hekta 44,000,000 kutoa
hekta 10,120,000). Ziada hii ya ardhi ambayo haitumiki kwa lolote inaonekana ni
kubwa sana. Hoja iliyoko mezani ni kuikodisha ardhi kwa wakulima wakubwa wa
kigeni kwa ajili kilimo cha mashamba makubwa ili serikali na wananchi wanufaike
na ardhi hii ambayo “haizalishi”.
Zinatolewa hoja kwamba wakulima wa kigeni
wataleta teknolojia ya kisasa na mitaji mikubwa itakayohuisha kilimo na kutoa
ajira kwa Watanzania. Kwamba “kupitia ukodishaji wa ardhi kwa wageni Tanzania
itafanya mapinduzi makubwa ya kijani na hatimaye kupunguza umaskini”.
Ni hoja tamu, na zimeongeza kasi zaidi katika
ukodishaji ardhi ili “tunufaike na kilimo cha kibiashara” ambacho kimsingi kipo
tokea tupate uhuru. Zinatolewa hoja kwamba “Watanzania wasiwe na wasiwasi kwani
ardhi ni mali ya taifa kwa mujibu wa Katiba na sheria.” Kwamba “mwekezaji
atakodishwa ardhi kwa muda wa miaka 33, 66 au 99 na baada ya hapo ardhi
itarejeshwa serikalini.” Hivyo basi “tuwapokee wakodishaji ardhi kwa mikono
miwili kwani wanaleta neema.”
Hoja hizi hazina mashiko kwani
zinahalalisha kurejeshwa kwa ukoloni kwa mgongo laini wa ukodishaji ardhi
jambo ambalo ni hatari sana kwa Tanzania ya leo na kesho na nitaeleza kwa nini.
Ukoloni unazo sura
nyingi sana na mbinu kila aina za kuliteka taifa. Ukodishaji ardhi ni njia
mojawapo ya kuukaribisha ukoloni mpya wa kutawaliwa na makampuni ya kibeberu.
Ukisema hili wanajibu kwamba “hizo ni fikira za kale -Tanzania ni nchi huru.”
Lakini ukweli unabaki
pale pale kwamba taifa-nchi (nation-state)
ni ardhi. Hivi taifa-nchi linakaa wapi? Unapoikodisha ardhi kwa miaka 99 ina
maana umeifanya ardhi hiyo kuwa ni koloni kwa miaka 99. Wajerumani na Waingereza
walitutawala jumla ya miaka 77. Katika miaka 99 na nguvu ya pesa, mlowezi
atafanya atakavyo. Na kwa kufanya hivi atakavyo Watanzania watageuzwa watumwa
ndani ya nchi yao. Watanyanyaswa na kupigwa viboko. Tunayashuhudia haya
yakifayika katika migodi ya dhahabu hadi Watanzania kuuwawa. Na katika Tanzania
inayokumbatia rushwa na ufisadi mwekezaji anakingiwa kifua.
Je Mtanzania kibarua
katika shamba la mlowezi atapata haki yake? Zipo taarifa nyingi kwamba kwa
kutumia rushwa wageni wanapewa ardhi bwerere. Na kwa mchakato uliopo wa uraia
wa nchi mbili (kama utapitishwa) katika siku si nyingi walowezi watapewa uraia
na Tanzania ya kesho itageuka kuwa Zimbabwe ya sasa. Watanzania wataidai ardhi
yao na walowezi wataiweka Tanzania katika msukosuko mkubwa.
Taarifa zinazohusiana na hizi:
http://muhunda.blogspot.com/2010/07/kaburi-la-mbaguzi-nambari-wani-cecil.html
Taarifa zinazohusiana na hizi:
http://muhunda.blogspot.com/2010/07/kaburi-la-mbaguzi-nambari-wani-cecil.html
Tuesday, January 8, 2013
Lugha yetu Kiswahili
Miaka mingi iliyopita wakati nafanya kazi Dar es Salaam nilikuwa natoa huduma ya kufasiri lugha ya Kitaliani kutoka kwenye nyaraka mbalimbali zenye maandishi ya Kiingereza na Kiswahili. Nilipata kusoma nchini Italia miaka mingi iliyopita ambako nilijifunza lugha ya huko.
Kwa kuwa mimi siyo mtaalamu wa lugha mara kadhaa nilitembelea ofisi ya Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) ambayo ilikuwa jirani na ofisi yangu ili kupata ufafanuzi wa maneno ambayo sikuwa na hakika niliyatumia kwa usahihi kwenye ile kazi ya tafsiri.
Wakati mmoja mtaalamu mmoja wa lugha huko BAKITA alinifahamisha kuwa maana sahihi kwa Kiingereza ya neno "tafsiri" ni translation na kuwa "kufasiri" ilikuwa na maana to translate. Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa maelezo yake, haikuwa sahihi kutamka: "Leo nimetafsiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza. Ilikuwa sahihi kusema: "Leo nimefasiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza. Hii ndiyo hoja yangu niliyokusudia kuiwasilisha leo hapa ambayo nimelazimika kuibadili baada ya kufungua kamusi ili kuhakikisha kuwa ninayotaka kuandika ni sahihi.
Nilichogundua ni tofauti kidogo na yale niliyoambiwa kule BAKITA. Ni kweli kuwa neno lina maana ile niliyofafanuliwa na yule mtaalamu. Lakini nimegundua sasa, kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili - Kiingereza toleo la 2001 iliyochapishwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ni sahihi pia kusema: "Leo nimetafsiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza."
Hisia zangi ni kuwa matumizi yasiyo sahihi yaliendelea kwa muda mrefu na kwa watumiaji wengi sana wa lugha ya Kiswahili na kuwafanya waandaaji wa Kamusi kuhalalisha matumizi mapya ya neno hilo.
Taarifa zinazohusiana na taarifa hii:
http://muhunda.blogspot.com/2010/10/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2012/11/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2010/04/lugha-yetu-kiswahili.html
Kwa kuwa mimi siyo mtaalamu wa lugha mara kadhaa nilitembelea ofisi ya Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA) ambayo ilikuwa jirani na ofisi yangu ili kupata ufafanuzi wa maneno ambayo sikuwa na hakika niliyatumia kwa usahihi kwenye ile kazi ya tafsiri.
Wakati mmoja mtaalamu mmoja wa lugha huko BAKITA alinifahamisha kuwa maana sahihi kwa Kiingereza ya neno "tafsiri" ni translation na kuwa "kufasiri" ilikuwa na maana to translate. Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa maelezo yake, haikuwa sahihi kutamka: "Leo nimetafsiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza. Ilikuwa sahihi kusema: "Leo nimefasiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza. Hii ndiyo hoja yangu niliyokusudia kuiwasilisha leo hapa ambayo nimelazimika kuibadili baada ya kufungua kamusi ili kuhakikisha kuwa ninayotaka kuandika ni sahihi.
Nilichogundua ni tofauti kidogo na yale niliyoambiwa kule BAKITA. Ni kweli kuwa neno lina maana ile niliyofafanuliwa na yule mtaalamu. Lakini nimegundua sasa, kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili - Kiingereza toleo la 2001 iliyochapishwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ni sahihi pia kusema: "Leo nimetafsiri aya mbili kutoka kwenye kitabu cha lugha ya Kiingereza."
Hisia zangi ni kuwa matumizi yasiyo sahihi yaliendelea kwa muda mrefu na kwa watumiaji wengi sana wa lugha ya Kiswahili na kuwafanya waandaaji wa Kamusi kuhalalisha matumizi mapya ya neno hilo.
Taarifa zinazohusiana na taarifa hii:
http://muhunda.blogspot.com/2010/10/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2012/11/lugha-yetu-kiswahili.html
http://muhunda.blogspot.com/2010/04/lugha-yetu-kiswahili.html
Monday, January 7, 2013
Miraji Mrisho Kikwete ateuliwa Makamu wa Rais wa IBF/Afrika Maendeleo ya Vijana
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
JANUARY
6, 2012
Shirikisho
la Ngumi la Kimataifa Afrika (IBF/Africa) limemteua Bw. Miraji Mrisho Kikwete
kuwa Makamu wa Rais anayeshughulikia maendeleo ya vijana katika bara la Afrika,
Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati. Uteuzi wa Miraji unaanza January mwaka
mpya 2013.
Katika
kumteua Miraji, Rais wa IBF katika bara
la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Bw. Onesmo Ngowi alisema kuwa Miraji ana uwezo wa
kuwahamasisha na kuwaunganisha vijana katika shughuli za maendeleo.
Aliendelea
kusema kuwa Miraji atakuwa anawahamasisha vijana, kuwaunganisha, kuwajengea
uwezo wa kimaendeleo yatakayoratibiwa na IBF.
Aidha, Rais
huyo alisema kuwa Miraji atakuwa anabuni njia mbalimbali za kuwaunganisha
vijana wa Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati ili waweze kufaidika na
miradi ya IBF ambayo inalenga kwenye elimu, kujenga vipaji pamoja na
kuwaunganisha kwenye biashara ya utalii wa michezo.
Katika
mkutano wake wa mwaka uliofanyika katika jiji la Honolulu, jimbo la Hawaii,
nchini Marekani hivi karibuni IBF iliupokea mradi wa “Utalii wa Michezo” uliobuniwa na kuwakilishwa na Rais wa IBF
katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtazania Onesmo
Ngowi.
Lengo kuu
la mradi huo ni kulifanya bara la Afrika, hususan Tanzania, kuwa kitovu kikuu cha
“Utalii Michezo” hivyo kujenga
uchumi imara. Nchi za Tanzania na Ghana ziliteuliwa kuwa nchi za mfano kwenye
mradi huo.
Katika
mradi huo, IBF itatumia mtandao ilionao katika nchi zaidi ya 203 duniani
kuhamasisha wanachama wake na famlia zao, wapenzi pamoja na marafiki zao kuja
Afrika/Tanzania kutalii pamoja na kuwekeza katika miradi mbalimbali.
Uteuzi wa
Miraji utasaidia kuwaunganisha vijana ili waweze kuchangia na kufaidika na
biashara ya utalii kwenye mradi huo na umefanywa wakati muafaka.
Miraji
ambaye ni mjasiriamali amejipambanua katika maendeleo ya jamii na ana mchango
mkubwa sana katika kuendeleza vijana nchini Tanzania.
Rais Ngowi
alimwelezea Miraji kama tegemeo ambalo vijana wanalihitaji kwani wanahitaji
uhamasishaji wa hali ya juu na Miraji ana uwezo wa kufanya kazi hiyo kwa
ufanisi mkubwa kwani alishawahi kuifanya kwa kipindi kirefu.
Miraji
Mrisho Kikwete ni msomi wa Chuo Kikuu cha nchini Oman ambako amesomea elimu ya
utawala wa biashara ambayo ndiyo lengo kuu la uteuzi wake. Ana haiba ya
kupendwa na vijana pamoja na uwezo wa kujichanganya nao.
Imetolewa
na:
Makao makuu
IBF Afrika, Ghuba ya Uajemi na
Mashariki ya Kati
Dar-Es-Salaam, Tanzania
Thursday, January 3, 2013
Taarifa ya Serikali kufafanua kuhusu miradi ya utafutaji na uvunaji wa gesi asilia nchini
****************************************************
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA NISHATI NA MADINI
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUFAFANUA KUHUSU MIRADI YA
UTAFUTAJI NA UVUNAJI WA GESI ASILIA NCHINI
1.0 UTANGULIZI
Wizara ya Nishati na Madini inapenda kutoa ufafanuzi wa miradi ya Gesi Asilia ambayo itatekelezwa kwa kushirikiana na wawekezaji katika Sekta
ndogo ya Gesi Asilia na kueleza manufaa makubwa yatakayopatikana kwa wananchi
wote wa Tanzania wakiwemo wale wa Mikoa ya Mtwara na
Lindi.
Siku
ya Alhamisi, tarehe 27 Disemba 2012, baadhi ya Vyama vya Siasa
vya Upinzani viliratibu na kuhamasisha baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara, wengi wao wakitokea Mtwara Mjini kufanya
maandamano ya kudai raslimali ya Gesi Asilia iwanufaishe wakazi wa Mtwara na kupinga mradi mkubwa wa ujenzi wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Mtwara hadi
Dar
es Salaam. Wizara ya Nishati na Madini inapenda kutoa taarifa
ifuatayo kwa Wa-Tanzania wote kwa kupitia
vyombo vya habari.
Tokea
Uhuru, uchumi wa Tanzania umetegemea kilimo cha mazao ya
biashara kama vile katani (Tanga na Morogoro), pamba (Mwanza, Mara
na Shinyanga), kahawa (Kilimanjaro, Kagera, Ruvuma na Mara), chai (Iringa) na tumbaku (Tabora). Fedha za mazao haya zimewanufaisha
wakazi wa mikoa yote ya nchi yetu bila ubaguzi wo wote wala wakulima
wa kutoka mikoa hiyo hawajawahi kufanya maandamano wakidai
upendeleo (dhidi ya Wa-Tanzania wengine)
wa aina yo yote ile.
1
Mapato yatokanayo na uchimbaji wa dhahabu (Mwanza, Geita, Mara, Shinyanga na Tabora), almasi (Shinyanga) na tanzanite (Manyara) yamewanufaisha Wa-Tanzania wote bila ubaguzi wo wote ule! Minofu ya samaki wa Ziwa Victoria (Mara, Mwanza na
Kagera) imeliingizia Taifa letu fedha nyingi ambazo zimetumiwa na wakazi wa nchi nzima bila ubaguzi
wo wote.
Aidha kuna mikoa ambayo inazalisha mazao ya chakula kwa wingi kwa
manufaa ya Wa-Tanzania wote. Mahindi kutoka Rukwa, Mbeya, Ruvuma na Iringa
yanasafirishwa kwenda mikoa yote ya nchi yetu bila kujali eneo
yanakolimwa na wakazi wa mikoa hiyo hawajawahi kudai mahindi hayo
ni kwa ajili
ya watu wa mikoa hiyo pekee. Sukari ya Kilombero, Mtibwa
na Kagera inatumiwa na wakazi wa mikoa yetu yote bila ya kuwepo madai ya mikoa inayozalisha sukari hii kupewa upendeleo wa
aina yo yote ile. Maji ya Mto Ruvu yanatumiwa na wakazi wa Dar Es Salaam bila
manung’uniko yo yote kutoka kwa wakazi wa eneo la chanzo cha Mto Ruvu.
Umeme wa kutoka Mtera, Kidatu na Kihansi (Dodoma na Morogoro),
Hale (Tanga), na Nyumba ya Mungu (Kilimanjaro) unatumiwa na wakazi wote wa Tanzania bila ubaguzi au malalamiko ya
wenyeji
wa sehemu ambazo umeme huo unafuliwa na kusafirishwa kwenye Gridi ya Taifa.
Kwa
hiyo, kutokana na mifano hii michache, ni wajibu wa wazalendo na
wapenda maendeleo wa kweli na hasa Wa-Tanzania wanaopinga ubaguzi
wa aina yo yote ile kujiuliza kwa kina sababu zilizopelekea Vyama Siasa
vya Upinzani kupanga, kuhamasisha, kushabikia na kuongoza
maandamano ya tarehe 27 Disemba
2012 pale Mtwara
Mjini.
2.0 RASLIMALI YA GESI
ASILIA TANZANIA
Gesi
Asilia ilianza kugundulika hapa nchini tangu mwaka 1974 kwenye Kisiwa
cha
Songo Songo, Mkoani Lindi.
Baada ya hapo
Gesi
Asilia imegundulika maeneo ya Mtwara Vijijini, yaani
Mnazi Bay (1982) na Ntorya (2012), Mkuranga (Pwani, 2007), Kiliwani (Lindi, 2008). Kiasi cha
Gesi Asilia iliyogunduliwa katika maeneo haya inakadiriwa kuwa Futi za
2
Ujazo Trilioni 4.5 – 8.
Katika
kipindi cha miaka mitatu iliyopita, kumekuwa na kasi kubwa ya utafutaji
Mafuta na Gesi Asilia uliojikita
zaidi kwenye maji
ya
kina
kirefu
cha
bahari. Kiasi cha Gesi
Asilia
iliyogundulika katika kina kirefu cha maji inafikia
takribani Futi za
Ujazo Trilioni 27. Kiasi cha wingi wa Gesi Asilia yote iliyogunduliwa
nchi kavu na baharini inafikia
takribani
Futi
za Ujazo Trilioni 35.
Kufuatana na Sheria
za
nchi yetu
zinazotumiwa
kugawa mipaka ya mikoa iliyopo kando
kando mwa bahari (isivuke 12 nautical miles au
22.22 km kuingia baharini), Gesi Asilia iliyogunduliwa hadi sasa katika
Mkoa wa Mtwara pekee ni asilimia 14 tu ya gesi yote iliyogundulika
nchini. Kwa kutumia
kigezo hicho cha Sheria za
mipaka ya
ki-utawala ya
mikoa yetu, Lindi inayo
7% ya gesi yote, Pwani
1% na huku Kina Kirefu cha Bahari (Deep Sea) ndicho chenye gesi nyingi (78%) kuliko mikoa
yote ikiwekwa pamoja! Kwa hiyo, hakukuwa na haja ya kufanya maandamano kwa sababu Gesi Asilia nyingi inapatikana kwenye bahari
ya kina kirefu ambayo iko
ndani ya mipaka ya nchi yetu bila kujali
mipaka ya mikoa yetu. Isitoshe Gesi Asilia imegundiliwa kwenye miamba
tabaka (sedimentary rocks) yenye umri wa Miaka kati ya Milioni 199.6
hadi 23.03. Mipaka ya Bara la Afrika, ya nchi yetu na ile ya mikoa yetu
haikuwepo
wakati huo!
Utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia pia unaendelea tukiwa wa mategemeo
makubwa ya
upatikanaji
wa
raslimali
hizi katika Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Manyara, Kigoma, Mbeya, Njombe,
Rukwa, Katavi,
Morogoro na Tabora pamoja na kwenye kina kirefu cha maji baharini kuanzia mpaka wetu na Msumbiji hadi mpaka wetu na Kenya. Hatutarajii mikoa hii nayo ifanye maandamano ya kutaka
kuhodhi
raslimali za Gesi Asilia na
Mafuta zitakapogunduliwa
mikoani
mwao.
3.0 MATUMIZI YA GESI ASILIA YA MNAZI BAY (MTWARA) NA
SONGO SONGO (LINDI)
Mpaka hivi sasa Gesi Asilia inayozalishwa na kutumika nchini ni kutoka
Mnazi Bay (Mtwara Vijijini) na Songo Songo (Kilwa, Lindi). Gesi ya Mnazi
3
Bay
kwa sasa huzalisha umeme kwa ajili ya Mikoa ya Mtwara na Lindi
tu. Mitambo ya kufua
umeme kutokana na Gesi Asilia iliyopo Mtwara Mjini inao uwezo wa kuzalisha MW 18 lakini
matumizi
ya umeme ya
Mikoa ya Mtwara na Lindi haijavuka MW 12. Umeme huo wa Mtwara
unafuliwa na TANESCO huku Kampuni za Wentworth na Maurel & Prom
zikizalisha Gesi Asilia (inayotumiwa na TANESCO) kiasi cha Futi za Ujazo Milioni 2 kwa siku. Ikumbukwe kwamba ufuaji wa umeme wa hapo Mtwara Mjini ulikuwa mikononi mwa Kampuni ya Artumas iliyofilisika. Tangu Desemba 2006 hadi leo hii kiasi cha gesi kilichotumika kufua umeme kwa ajili ya mikoa hiyo miwili ni chini ya asilimia 1 ya gesi yote iliyogundulika Mnazi Bay (Mtwara Vijijini).
Vilevile ikumbukwe kwamba kuna
visima
vinne vya Gesi
Asilia
pale Mnazi Bay (Mtwara Vijijini) na kinachotumika kwa sasa na tena kwa
kiwango cha chini kabisa ni kimoja tu!
Aidha ni vizuri
ndugu zangu Wa-Tanzania wakaelewa kuwa Gesi Asilia hii inatafutwa na kuchimbwa na wawekezaji wenye
mitaji mikubwa,
wataalamu na teknolojia ya utafutaji na uchimbaji wa Gesi Asilia ambao wanapaswa kurejesha mitaji yao. Uchorangaji wa kisima kimoja cha
utafutaji wa Gesi Asilia nchi kavu unahitaji Dola za Marekani Milioni
40, na kwenye kina kirefu cha maji baharini zinahitajika zaidi ya Dola za Marekani Milioni 100. Ikumbukwe kwamba, Serikali kwa
kushirikiana na Shirika la Mafuta la Tanzania (TPDC), inatumia fedha za
walipa kodi wa nchi nzima kwa shughuli za kuvutia, kuratibu na
kusimamia utafutaji na uendelezaji wa Gesi Asilia nchini kote ikiwemo
Mikoa ya Mtwara na Lindi. Walipa kodi Wa-Tanzania bado hawajalalamika wala hawajafanya maandamano ya kudai fedha zao za kodi
zisitumike huko
Mtwara!
Ni muhimu pia tukaelewa kwamba Gesi Asilia iliyopo Mnazi Bay (Mtwara Vijijini) inazalisha umeme
peke yake kwa ajili ya Mikoa ya Mtwara na Lindi. Gesi Asilia ya Songo Songo (Kilwa, Lindi) ndiyo inayotumika kuzalisha umeme kwa ajili ya Gridi ya Taifa, na pia kwa ajili ya
wananchi wa Kisiwa
cha
Songo Songo (Lindi),
maeneo ya Somanga
4
Fungu (Lindi) na viwandani (Dar Es Salaam). Tangu Oktoba 2004 ambapo mitambo ya kufua umeme ilipoanza kazi hadi leo hii, kiasi cha Gesi Asilia ya Songo Songo kilichotumika ni asilimia 7 tu ya Gesi Asilia yote iliyogunduliwa huko. Kwa hiyo, takwimu zinaonyesha kwamba hata
uchumi wa Jiji la Dar Es Salaam unatumia kiasi kidogo sana cha Gesi
Asilia (7%) iliyopo Songo
Songo
(Kilwa,
Lindi).
Ikumbukwe kwamba
waajiriwa kwenye viwanda vya Dar Es Salaam wamo wanyeji wa kutoka
Mtwara Mjini ambako maandamano yalifanyika na vilevile wamo
wafanyakazi ambao ni wanachama wa Vyama vya Siasa
vya Upinzani vilivyopanga, ratibu na kushabikia maandamano ya Mtwara Mjini ya tarehe
27
Disemba 2012.
4.0 MIPANGO YA MATUMIZI YA GESI ASILIA KATIKA KIPINDI CHA
MIAKA 5 HADI 10
(a) Ujenzi wa
Bomba
la Gesi Asilia hadi Dar Es Salaam:
Kuuza Gesi Asilia Jijini Dar es Salaam, kitovu cha uchumi wa
Tanzania (80% ya mapato ya nchi yetu yanazalishwa Dar Es Salaam) ni uamuzi mzuri wa ki-uchumi. Tayari kuna viwanda
34 vinatumia Gesi Asilia
ambavyo vinahitaji kupanua shughuli zao endapo gesi zaidi
itapatikana. Soko kubwa la Gesi Asilia
lipo tayari Dar es Salaam (na siyo Mtwara), ambapo ipo
mitambo ya kufua umeme kwa kutumia mafuta. Serikali
inatumia fedha nyingi za kigeni kununulia mafuta ya kufua
umeme tunaoutumia kila siku. Takribani Dola za Marekani Bilioni Moja (sawa na Shilingi Trilioni 1.6) kwa mwaka
zitaokolewa kutokana na mitambo iliyopo nchini ikifua umeme
kwa
kutumia Gesi Asilia na kuachana na mafuta ambayo ni ya
bei
kubwa sana.
Bei
ya
umeme kwa
uniti
moja (KWh)
ya
umeme unaofuliwa kutumia dizeli na mafuta ya aina nyingine ni kati ya Senti za Marekani 30 hadi 45 na huku bei ya uniti
moja
hiyo hiyo ni Senti za Marekani 6-8 kwa umeme utokanao na Gesi Asilia na
zinapungua na
wakati wa matumizi.
Vilevile, takribani Dola za Marekani millioni 202 kwa mwaka zitaokolewa iwapo Jiji la Dar Es Salaam litatumia Gesi Asilia badala ya mafuta katika magari, taasisi na majumbani. Fedha
5
hizi zikiokolewa zitatoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa
Taifa letu kwa manufaa ya Wa-Tanzania wote wakiwemo wale waliondamana na wale walioratibu maandamo ya Mtwara Mjini ya tarehe
27
Disemba 2012.
(b) Umeme mwingi
zaidi
kutokana na
Gesi Asilia:
Bomba la Gesi Asilia linalojengwa litasafirisha gesi nyingi zaidi
ambayo itawezesha mitambo mipya itakayojengwa Kinyerezi (Dar
Es Salaam) kufua
umeme wa zaidi ya MW
990.
Umeme mwingine utafulia Somanga Fungu
(Lindi) wa kiasi
kisichopungua
MW
520.
(c) Usafirishaji na
usambazaji wa
umeme nchini mwetu:
Dar es Salaam ndiko kuna miundombinu mikubwa ya
usafirishaji na
usambazaji wa umeme
kuliko mikoa mingine
yote, hivyo ni uamuzi wa ki-uchumi unaotulazimisha kusafirisha Gesi Asilia kutoka Mikoa ya Lindi na Mtwara na kuipeleka Dar Es Salaam ambako itatumika kufua umeme, na kutumika moja kwa
moja
viwandani, majumbani na
kwenye magari.
(d) Kwa
kuzingatia mahitaji
ya Gesi
Asilia yatakayojitokeza:
Bomba la kusafirisha gesi litawekewa matoleo ya kuchukulia gesi
(tie-off) katika maeneo ya Mtwara, Lindi, Kilwa na Mkuranga
ili kuhakikisha kuwa miji hii inakuwa na Gesi Asilia ya uhakika
wakati wowote itakapohitajika. Kwa hiyo kuweka mitandao ya
usambazaji wa gesi kutoka kwenye Bomba la Gesi Asilia
linalojengwa kutarahisisha
matumizi ya Gesi Asilia viwandani na
majumbani katika Mikoa ya Mtwara na Lindi, na kwenye mikoa mingine kwa siku za
baadae.
(e)Serikali imetenga maeneo katika pwani ya Mikoa ya Kusini
(Lindi na Mtwara) kwa ajili ya uanzishwaji wa maeneo ya
viwanda (Industrial Parks/Estates) vikiwemo viwanda vya
mbolea, Liquefied Natural Gas (LNG) na Petrochemicals. Ujenzi wa kiwanja cha sementi uko katika hatua za mwisho za
maandalizi.
(f) Ili kutengeneza mazingira mazuri ya biashara ya Gesi Asilia na
Mafuta kwa kampuni za huduma, malighafi na vitendea kazi,
Serikali imetenga eneo maalumu Mtwara,
ambalo
litawekewa
6
miundombinu ya msingi ili kutoa vivutio mbalimbali kwa
makampuni hayo. Eneo hilo litapewa hadhi ya Ukanda Huru wa
Bandari (Freeport Zone).
Ni
lazima shughuli za kusafisha na kusafirisha Gesi Asilia zitatoa ajira
katika
maeneo
husika. Kwa
mfano kwa
mitambo ya
kusafishia
gesi
inayojengwa Madimba (Mtwara Vijijini) na SongoSongo (Kilwa, Lindi), kila mtambo utahitaji wafanyakazi na wengine watatoka Mikoa ya Lindi na
Mtwara.
Watanzania wanakumbushwa kuwa
raslimali zilizopo nchini ikiwemo
gesi asilia, madini, makaa ya mawe, wanyama pori, misitu, milima ya
utalii, mito, maziwa, bahari n.k ni za Wa-Tanzania wote kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Raslimali hizi
zinapatikana, zinatunzwa na kuzalishwa maeneo mbalimbali nchini
mwetu na mapato yake yanatumika kwa maendeleo ya Wa-Tanzania wote
bila
kujali maeneo raslimali
hizo zilipo.
Tusikubali kuvunja nchi yetu vipande vipade kwa kisingizio cha raslimali zilizopo mikoani
mwetu. Tusikubali kuvunjavunja mikoa yetu kwa kisingizio cha raslimali zilipo kwenye wilaya zetu.
Tusikubali kuvunjavunja wilaya zetu kwa kisingizio cha raslimali
zilizopo kwenye tarafa zetu. Tusikubali kuvunjavunja tarafa zetu kwa kisingizio cha raslimali zilizopo kwenye kata zetu. Tusikubali
kuvunjavunja kata zetu kwa kisingizio cha raslimali zilizopo kwenye
vijiji vyetu na
mitaa
yetu.
MUNGU
IBARIKI TANZANIA, DUMISHA UHURU NA UMOJA WETU
Prof Dr Sospeter Muhongo (Mb)
WAZIRI YA NISHATI NA MADINI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
7
Subscribe to:
Posts (Atom)